I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, May 28, 2010

ZANZIBAR:

Mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na utawala bora Tanzania Jaji mstaafu Amir Ramadhani Manento ameonya masuala ya rusha katika uchaguzi mkuu ujao yanaweza yanaweza kulinagamiza taifa endapo halitadhibitiwa.
Akifungua mkutano wa baraza la tume hiyo mjini hapa amesema madhara ya rushwa katika uchaguzi yanaweza kuleta ubinafsi kwa viongozi watakaochaguliwa hivyo halina budi kupigwa vita kwa nguvu zote.
Jaji Mamento amehimiza kuelimishwa kwa wananchi haki yao ya kuchagua au kuomba kuchaguliwa bila kushwishiwa ili kuepusha vitendo vya rushwa katika uchaguzi huo…
Mkutano huo wa tisa wa baraza la tume ya haki za binadamu unahusisha wawakilishi kutoka vyama vya wafanyakazi na baraza kuu la wafanyakazi serikalini.

1 comment: