I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 4, 2010

VIWANJA VYALETA UTATA

Mzozo wa upimaji wa viwanja katika shehia ya Pwani mchangani umeibuka tena baada ya wananchi wa shehia hiyo kuja juu na kusema hawakushirikishwa na kutoridhika na upimaji huo.
Wakizungumza na mwandishi wetu katika kijiji hicho wamesema hali hiyo inaashiria kuwepo nia ya kutaka kunyanganywa viwanja vyao bila ya wao kushirikishwa.
Wamesema katika upimaji huo kumefanyika ujanja ili kunyimwa haki zao na kuitaka serikali kuu kuingilia kati juu ya mzozo huo
Migogoro ya ardhi imekuwa ikiibuka mara kwa mara hasa katika maeneo ya ukanda wa utalii kutokana na maeneo ya ardhi katika sehemu hizo kuuzwa kwa bei kubwa kwa watu wanaokeza katika maeneo hayo.

No comments:

Post a Comment