I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 2, 2010

ABIRIA WAZILALAMIKIA MELI ZA ABIRI ZANZIBAR

Vyombo vya usafiri wa majini vya abiria vinavyofanya safari kati ya Dar es salaam na Zanzibar vimelalamikiwa na wananchi wa Zanzibar kutokana na tabia ya kujaza abiria kupita kiasi na kutishia usalama wa abiria.

Akizungumza na Zenj Fm radio juu ya malalamiko hayo mrajisi wa meli Zanzibar Abdalah Mohamed amesema meli zinazofanya safari kati ya Dar es salaam na Zanzibar zimekuwa zikikaguliwa mara kwa mara.

Amesema meli hizo zinapokuja Zanzibar kabla ya kusajiliwa ni lazima ikaguliwe na kufuata taratibu zote za huduma za usafiri wa baharini ili zipewe kibal.

Akizungumzia suala la uzidishaji wa abiria ambalo linaonekana kutokea mara kwa mara amesema meli kikawaida inaweza kuzidisha abiria kutokana na sababu maalum ikiwemo wakati wa sherehe.

Hivi karibuni meli ya Flying Hourse iliripotiwa kuzidisha abiria ikiwa katika bandari ya Malindi ambapo abiria waliokuwa katika meli hiyo walipata hofu na hivyo kulazimika kurudi tena bandari wakati nahodha wa meli ya Sea Bus alipandishwa mahakamani kwa kosa kama hilo.

No comments:

Post a Comment