I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 6, 2010

HOSPITALI YA CHAKECHAKE WALIA NA UKOSEFU WA DAMU UNAOPELEKEA KUKWAMISHA UPASUAJI


Hospitali ya ChakeChake walia na Ukosefu wa damu unaopelekea kukwamisha Upasuaji
Kufuatia kuwepo kwa taarifa za Wodi ya watoto ya Hospitali ya Chakechake kutokuwa na huduma za matibabu ikiwemo dawa na mashuka ,daktari wa zamu nyakati za usiku pamoja na damu ya akiba ambayo inakwamisha upasuaji mkubwa.

Jitihada za Mwangaza wa habari kuweza kupata taarifa za kina kuhusiana na matatizo yanayoikabili hospitali hiyo, tulimtafuta katibu wa Hospitali ya Chake Chake Abushiri Masoud na alipoulizwa juu ya tatizo hilo.Bonyeza Hapa kumsikia
Katibu wa Hospitali ya Chake Chake Abushiri Daudi
Mwangaza wa habari haukuishia hapo ulimtafuta Daktari wa upasuaji wa Hospitali hiyo ya Chakechake Dk.Shaaban Issa Mohamed, kutokana na madai kuwa hospiatli hiyo inakabiliwa na tatizo la uapasuaji kutokana na ukosefu wa akiba ya damu.
Dk.Shaaban amekiri kuwepo kwa tatizo hilo la ukosefu wa damu katika Hospitali hiyo ,ambapo hulazimu kwenda mpaka Wete ambapo pia hukosa huduma hiyo ya damu.Bonyeza hapa kumsiia
Dk.Shaaban Issa Mohamed
Baada ya kubainika kwa tatizo hilo la ukosefu wa damu huko Pemba,Mwangaza umezungumza na Afisa uhamasishaji Mpango wa Taifa wa Damu salama Zanzibar Omari Said Omar ili kujua kama kitengo chao kinafahamu kuhusiana na tatizo hilo ambalo linaendelea huko Pemba la upungufu wa damu hususan katika hospitali hiyo ya ChakeChake.Bonyeza hapa kumsikia
Omari Said Omar Afisa uhamasishaji Damu

No comments:

Post a Comment