I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 11, 2010

SEIF HATIB AJIBU SHUTUMA


Baadhi ya vyombo vya habari vimedai kuwa viongozi wa Jimbo la Uzini kwa kipindi cha maika mitano wamekuwa wakitoa ahadi hewa kwa wananchi wa jimbo hilo jambao ambalo limepelekea wananchama 50 wa CCM kurudisha kadi zao.
Vyombo hivyo vimeendelea kwa kudai kuwa wanachama hao wameamua kurudisha kadi hizo vikimtuhumu mbunge wa jimbo hilo Mh Mohd Seif Khatib kuwa hajatekeleza ahadi zake.
Kufuatia madai hayo Mwangaza wa Habari ulitaka kufahamu kiini cha tokeo hilo kwa kuzungumza na baadhi ya wahusika wa kadhia hiyo.
Miongoni mwa wananchi waliorudisha kadi zao ambae pia ni mkaazi wa Umbuji katika jimbo la Uzioni ni B w Hassana Abdalla umaarufu Kunguru ambae amekiri kurudisha kwa kadi yake ya uanachama ya CCM lakini amesema kuwa hawakurudisha kadi hizo kwa kumshinikizo mbunge wao na badala yake waliamua kuishinimiza Serikali kuu kwa vile ilitoa ahadi.
Aidha Bw Hassan amekanusha kuwa walijitoa moja kwa moja katika chama cha mapinduzi na kusema kuwa waliamua kupumzika hadi hapo ahadi itakapotekelezwa ambapo kwa sasa mambo yameshasawazishwa..bonyeza HAPA kumsikia Bw.. Hassan Abdalla ....Miongoni mwa wakaazi wa Umbuji waliorejesha kadi
Baada ya kumsikia mkaazi huyo tulimtafuta Mwenyekiti wakamati ya wazee wa Umbuji, Mzee Kassim Mohd Haji ambae nae alikanusha taarifa hizo na kusema yafuatayo...Clip.... Kassim Mohd Haji....Mwenyekit wa wazee wa Umbuji
Mwangaza hakuishia hapo bali pia ulizungumza na katibu wa CMM Jimbo la Uzini Bw Mzee Rajab Vuai ambae amekanusha vikali madai hayo ya vyombo vya habari kuwa jimbo hilo kwa muda mrefu halina maendeleo yoyote chini ya mbunge na mwakilishi wa sasa.
Bw Rajab amesema kuwa wanachama hao hawakujitoa kabisa ndani ya CCM na baadhi yao kazi zao zilirudishwa na watoto wao..Bonyeza HAPA kumsikia.. Katibu wa CCM jimbo la Uzini
Baada ya kumsikia katibu wa CCM jimbo la Uzini kuhuisiana na kadhia hiyo, tulimgeukia Mwenyekiti wa CCM wilaya ya kati Bw Hassan Shaaban atuthibitishie taarifa za wanachama hao kurudisha kazi zao ambapo alilithibitisha hilo na kusema kuwa sababu kubwa ya wananchi hao ni kushindwa kutekelezwa kwa ahadi ya rais ya kuwajengea barabara ya lami..Bonyeza HAPA kumsikia Mwenyekiti wa CCM wilaya ya kati
Tulikata mzizi wa fitina kwa yote tuliyasikia kwa kumtafuta Mbunge wa jimbo la Uzini ambae pia ni waziri wan chi ofisi ya makamo wa Rais Muungano Mh Mohd Seif Khatib ambae anatoa ufafanuzi juu ya kile kilichodaiwa na baadhi ya vyombo hivyo vya habari..Bonyeza HAPA kumsikia Mh Mohd Seif Khatib...Majibu ya kutojenga bara bara

No comments:

Post a Comment