I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 23, 2010

ZANZIBAR:

Jaji wa mahakama kuu ya Zanzibar Mshibe Ali Bakar ameonya juu ya vitendo vya uvunjaji wa sheria vinavyoendelea kutokea siku hadi siku hapa Zanzibar.
Akizundua ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2009 mjini hapa amesema ripoti hiyo inahitaji kufanyiwa kazi ili kuona yale yaliotokea katika mwaka huo ikiwemo uvunjaji wa haki za binadamu hayatokei tena.
Amesema vitendo vya uvunjaji wa sheria vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara katika maeneo yote nchini na kutishia amani ya nchi, hivyo ni vyema kwa taasisi husika kuifanyika kazi ripoti hiyo.
Mshibe amesema nchi kadhaa zimepata mafanikio katika kupunguza vitendo vya uvunjaji wa sheria na haki za binadamu kutokana na ripoti kama hizo, hivyo ni vyema kuwepo na ufuatiliaji wa ripoti hiyo.
Ripoti hiyo iliyoandaliwa na kituo cha huduma za sheria Zanzibar pamoja na mambo mengine inazungumzia ukosefu wa ushahidi katika undelezwaji wa kesi.

No comments:

Post a Comment