I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 4, 2010

WANAFUNZI NDIO WANAO ATHIRIKA NA KICHOCHO


Kitengo cha kichocho, minyoo na Matendo kimesema tatizo la kichocho limekuwa likiathiri zaidi wanfunzi kutokana na baadhi ya skuli kutokuwa na huduma ya vyoo.Hayo yameelezwa na Meneja a kitengo hicho Khalfani Abdallah Mohammed wakati akizungumza na zenji Fm radio huko afisni kwake Mianzini Lumumba mjini Zanzibar.Amesema Kutokana na hali hiyo kitengo hicho kwa kushirikiana na wizara ya elimu na kitengo cha mazingira itafanya tathmini juu ya tatizo hilo pamoja na kutoa dawa za ugonjwa huo…Amefahamisha kuwa maradhi ya kichocho yamekuwa yakikabili wiliya zote za Pemba na Mkoa wa kaskazini Unguja,Wilaya ya kati na Wilaya ya Magharib na baadhi ya maeneo ya wilaya ya mjini…Hivyo amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanawakataza watoto wao kutochezea maji machafu ambayo yanaweza kusababisha maradhi hayo.

No comments:

Post a Comment