I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 20, 2010

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR IMETOA MSAADA WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 27

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetoa msaada wa zaidi ya shilingi milioni 27 kusaidia watu waliopatwa na maafa ya kubomokewa na nyumba zao kufuatia upepo uliovuma miezi kadhaa katika shehia za Kilimahewa, Kwamtipura na Amani.
Akikabidhi hundi yenye tahamani ya fedha hizo kwa mkuu wa mkoa wa mjini magharibi waziri wanchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma amesema serikali kwa kujali wananchi kutokana na hasara walioipata imeona ipo haja ya kuwafariji kwa msaada wa fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari waziri Hamza amesema fedha hizo zimetolewa baada ya kamati maaluma iliyounda kutahmini maafa hayo na kuitaka afisi ya mkuu wa mkoa kuhakikisha fedha hizo zinawafika walengwa.
Akipokea hundi hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa mjini Magharin afisa tawala wa Mkoa huo Amour Haji Nassor amewapongeza wnanchi walipata maafa hayo kwa ustahamilivu wao
Kiasi ya nyumba 74 ziliharika baada ya kuzuka upepe mkubwa katika maeneo ya Kilimahewa ,Kwamtipura na Amani

No comments:

Post a Comment