I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, May 21, 2010

KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM YUSSUF MAKAMBA AMESEMA


Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi CCM Yussuf Makamba amesema maandalizi ya mkutano mkuu wa chama hicho utakaomchagua mgombea urais wa Tanzania yanaendelea vizuri.
Akizungumza na Zenji Fm radio kuhusiana na kikao cha kamati kuu kilichofanyika jana mjini Dar es Salaam amesema mkutano huo utakaofanyika July 10 na 11 mjini Dodoma pia utapokea ratiba ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi, kupitisha mwelekezo wa CCM 2010-2020 na kupokea taarifa ya uchaguzi ya 2010-2015.
Aidha Makamba amesema mkutano huo utateuwa majina ya wagombea kupitia chama hicho katika nafasi za udiwani, uwakilishi na ubunge kwa majimbo yote ya Tanzania bara na Zanzibar

No comments:

Post a Comment