I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, May 10, 2010

MAMA SALMA KIKWETE


Mwenyekiti wa Mfuko wa taasisi ya wanawake na maendeleo WAMA Mama Salma Kikwete ameitaka jamii kupanga mikakati ya kukabiliana na na matatizo wanayokabili wanafunzi wa kike ikiwemo mimba za umri mdogo.
Amesema hayo wakati akizungumza na wanafunzi alipofanya ziara maalum ya kuangalia maendeleo ya wanafunzi wa kike na kuwahimiza umuhimu wa elimu katika skuli ya sekondari ya Benbella mjini Zanzibar.
Amesema wanafunzi wengi wanakabiliwa na changamoto za ndoa za umri mdogogo, ubakaji na tatizo la umasikini katika familia.
Amesema matatizo hayo yamekuwa yakisababisha kurudisha nyuma maendeleo ya wanafunzi wa kike katika kujikomboa kielimu…
Mama Salma pia amewataka wanafunzi wa kike kujitokeza zaidi na kukabiliana na ushindani wa kimasomo hasa katika masomo ya sayansi kwani taifa linahitaji wataalamu wazuri.
Nae mwalimu mkuu waskuli ya sekondari BenBela Asia Iddi amesema skuli hiyo ina idadi kubwa ya wanafunzi ikilinganishwa na uchache wa madarasa ya kusomea na walimu.

No comments:

Post a Comment