I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 4, 2010

TUCTA HATIMAE IMESITISHA MGOMO WA WAFANYAKAZI


Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA limisitisha mgomo wa wafanyakazi wa nchi nzima uliokuwa uanze leo baada ya serikali kusema mgomo huo sio halali.
Akizungumza na Zenji Fm radio mwenyekiti wa TUCTA Omar Ayoub amesema wameamuwa kusitisha mgomo huo kwa madai ya kuwepo mazingira ya hatari endapo wafanyakazi watagoma
Aidha mwenyekiti huyo amewataka wafanyakazi wote nchini kuwa na subira huku wakisubiri matokeo ya mkutano utakaofanyika kati ya TUCTA na serikali tarehe nane mwezi huu ambao unaweza kuleta matokeo mazuri Shirikisho hilo lilitaka kuitisha mgomo wa wafanyakazi wa nchi nzima kudai nyongeza za misharaha ya kima cha chini kufikia zaidi ya shilingi laki tatu, kupunguza kodi wanazokatwa wafanyakazi katika mishahara yao na kuitaka serika ihakikishe mifuko ya hifadhi ya jamii inatoa mfao mazuri.

No comments:

Post a Comment