I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, November 1, 2010

DR SHENI ASHINDA KITI CHA URAIS ZANZIBAR

HAYAA WADAU MUDA MFUPI TUU TAYARI MATOKEO YA KURA ZA UCHAGUZI ZNZ ZIMEKWISHA KAMILIKA . MUDA MFUPI TU TUME IMEMTANGAZA DR SHENI KUWA NDIE ALIYE SHINDA KITI CHA URAIS ZNZ

HABARI KAMILI INAKUJA SOON

WAKATI WOWOTE KUTOKA SASA TUTAPATA KUMJUA RAIS MPYA WA ZNZ

Umati mkubwa wananchi umekusanyika mbele ya kituo cha kutangazia matokeo ya uchaguzi katika hoteli ya Bwawani wakiisindikiza tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika juzi yatolewe haraka badala ya kutangazwa kwa utaratibu wa kusuasua.

Wananchi hao walijaa ndani ya hoteli na ukumbi wa salama wa hoteli hiyo huku baadhi yao wakiwa nje ya geti ambapo jeshi la polisi lililazimika kufunga lango na kuwazuwia baadhi yao wasiingie ndani kutokana na kuwa ndani ya hoteli hiyo kulijaa umati mkubwa wa watu .

Vijana na akina mama walikuwa wengi katika lango la hoteli hilo huku wakiimba na nyimbo huzuni na kusoma quran tukufu na kumshitakia Mwneyenzi Mungu kwa kuomba dua za kumhifadhi Maalim Seif na balaa na kuitakia kheri Zanzibar na watu wake katika kipindi hiki cha utangazaji wa matokeo.

Jeshi la polisi jana lilionekana likifanya kazi kubwa na kuhakikisha usalama unapatikana katika eneo lote la hoteli hiyo ikiwa pamoja na kuwasogeza wafuasi hao wakiwataka wakae chini huku magari ya maji ya kemikali na polisi waliovalia kivita wakiwa pembeni kwa wafuasi hao.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wamesema hawataandoka maeneo hayo hadi hapo tume ya uchaguzi itakapotangaza matokeo ya urais kwani imekuwa ukichelewesha kwa makusudi na kuishutumu tume hiyo kwamba inataka kubadilisha matokeo halisi yaliokusanywa vituoni.

“Hapa hatutaondoka mpaka tusikie rais akitajwa maana huu ni uchaguzi wane unafanyika nchini kwetu lakini imekuwa kawaida kukawilishwa matokeo lakini sisi tunachotaka ni kutangazwa kwa matokeo na sio jambo jengine” alisema Asha Abdallah ambaye ni miongoni mwa akina mama waliokuja na watoto wake.

Wananchi hao ambao wengi wao wanaonekana ni wafuasi wa chama cha wananchi (CUF) wamesema wasingependa kufanya fujo wala kusababisha madhara kwa mwengine lakini kwa kuwa wanataka maoni yao yaheshimiwe hawana budi kutetea haki yao ambayo imekuwa ikiporwa kwa muda mrefu na watawala.

“Mtatusamehe sana waandishi wa habari na waangalizi sisi tumekuja hapa sio lengo letu kufanya fujo lakini lengo letu ni kuwa mawazo yetu na maamuzi yetu tulioamua ndani ya kisanduku cha kura tunataka yaheshimiwe na watawala kwa hivyo tunataka ushindi wa maalim seif apewe mwenyewe haraka..tunachotaka maalim seif atangazwe maana matokeo yanaonesha yeye anaongoza akifuatiwa na Dk Shein” alisema Hassan Hamad Nassor.

Tokea juzi tume ya uchaguzi Zanzibar kupitia mwenyekiti wake, Khatib Mwinyichande imekuwa ikitoa matokeo ya urais huku matokeo ya uwakilishi, udiwani na ubunge yakitolewa majimboni.

Kwa mujibu wa Khatib hadi sasa CUF imepata majimbo matatu kwa upande wa Unguja ikiwemo jimbo la Mji Mkongwe, Magogoni na Mtoni huku majimbo mengine mengi yaliotangazwa yakishikiliza na CCM ikiwemo la Donge na Uzini ambayo yameshinda kwa zaidi ya asilimia 90

WAGOMBEA UWAKILISHI NA UBUNGE KUTOKA CUF WAMESHINDA MAJIMBO YA PEMBA

Wagombea wa nafasi za uwakilishi na ubunge Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF wanaendelea kushinda katika majimbo mbali mbali kisiwani Pemba.

Matokeo ya hivi karibuni mgombea uwakilishi jimbo la Tumbe kwa tiketi ya CUF Rufai Said Rufai ameshinda jimbo hilo kwa kupata kura elfu tano 312 na kumshinda mpinzani wake wa karibu wa CCM Amour Khamis Mbarouk aliepata kura 470.

Matokeo ya ubunge jimbo la Mkoani Ali Khamis Seif wa CUF ameshinda jimbo hilo, jimbo la Mkanyageni Mohamed Habib Mnyaa wa CUF ameshinda jimbo la Mtambile mgomea wa CUF Masoud Abdala Salum ameshina ubunge jimbo hilo.

Jimbo la Kiwani mgombea ubunge wa CUF Abdala Haji Ali meshanda wa jimbo hilo, jimbo la Chambani mbunge ni Salum Hemed Khamis wa CUF. Mwandishi wetu Haji Nassoro kutoka Pemba

Na huko jimbo la Wawi mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CUF Hamad Rashid Mohame ameshinda kwa kupata kura elfu tano 321 na kumshinda mpinzani wake karibu kutoka CCM Daud Khamis Juma aliepata kura elfu mbili 255

KAZI ZA KUHESABU KURA ZA RAIS WA TANZANIA ZINAENDELEA KUHESABIA

Kazi za kuhesabu kura kwa ajili uchaguzi wa urais wa jamhuri ya muungano Tanzania zinaendelea katika maeneo mbali mbali hasa yale ya Tanzania bara.

Hata hivyo baadhi ya maeneo ya Zanzibar kazi za kuhesabu kura zimalizika na kinachosubiriwa ni kutangazwa kwa matokeo ya jumla ya tume ya taifa ya uchaguzi NEC.

Waangalizi wa kimataifa wamesema kazi za upigaji kura zilifanyika kwa amani na utulivu licha ya kujitokeza kasoro ndogo ndogo.

Mkurugenzi wa tume ya taifa ya uchaguzi NEC Rajab Kiravu amesema uchaguzi wa majimbo yakiwemo majimbo manne ya Zanzibar umeahirishwa kutokana na upungufu wa karatasi za kupigia kura.

Amesema uchaguzi huo utarejewa tena Novemba 14 mwaka huu

MATOKEO YA URAIS MAJIMBO YA PEMBA

ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.

WAWI
CCM 2024 25.0%,
CUF 6,036 74.4%,
AFP 13 0.2%,
JAHAZI ASILIA 11 0.1%,
NCCR MAGEUZI 12 0.1%,
NRA 7 0.1%,
TADEA 6 0.1%.

CHONGA
CCM 2,150 34.1%,
CUF 4,108 65.2%,
AFP 10 0.2%,
JAHAZI ASILIA 16 0.3%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%,
NRA 6 0.1%,
TADEA 3 0.0%.

OLE
CCM 8,93 13.7%,
CUF 5,775 86.2%,
AFP 6 0.1%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 4 0.1%,
NRA 6 0.1%,
TADEA 5 0.1%.

CHAKE
CHAKE CCM 1,575 21.9%,
CUF 5,530 77.7%,
AFP 12 0.2%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 2 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

MTAMBWE
CCM 307 5.4%,
CUF 5,415 74.4%,
AFP 1 0.0%, JAHAZI
ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 2 0.0%,
NRA 3 0.1%,
TADEA 4 0.1%.

KONDE
CCM 6,53 10.1%,
CUF 5,751 89.9%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 10 0.1%,
NCCR MAGEUZI 10 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

MTAMBILE
CCM 961 16.1%,
CUF 4,9818 83.5%,
AFP 3 0.1%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 5 0.1%,
TADEA 6 0.1%.

WETE
CCM 1,159 25.5%,
CUF 6,317 83.3%,
AFP 1 0.0%, JAHAZI
ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%, NRA 2 0.0%, TADEA 2 0.0%.

KOJANI
CCM 562 8.2%,
CUF 6,262 91.5%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 3 0.0%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 1 0.0%.

GANDO
CCM 8,84 14.4%,
CUF 5,239 85.4%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 8 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

MGOGONI
CCM 615 9.8%,
CUF 5,614 89.1%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 12.0%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 3 0.0%,
TADEA 0 0.0%.


ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.

ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.


KONDE CCM 6,53 10.1%,
CUF 5,751 89.9%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 10 0.1%,
NCCR MAGEUZI 10 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

WETE CCM 1,159 25.5%,
CUF 6,317 83.3%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%,
NRA 2 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

KOJANI CCM 562 8.2%,
CUF 6,262 91.5%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 3 0.0%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 1 0.0%.

GANDO CCM 8,84 14.4%,
CUF 5,239 85.4%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 8 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

MGOGONI CCM 615 9.8%,
CUF 5,614 89.1%, AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 12.0%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 3 0.0%,
TADEA 0 0.0%

MATOKEO YA URAIS MAJIMBO 22 YA UNGUJA

TUME ya uchaguzi Zanzibar imetangaza matokeo ya awali ya nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa majimbo 18 ya Unguja na mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha mapinduzi CCM DK ALI MOHAMED SHEIN ameonekana kung,aa zaidi kwa ushindi wa majimbo mengi kisiwani Humo.
Akisoma matokeo hayo mbele ya waandishi wa habari,waalikwa,waangalizi wa uchaguzi na wananchi katika ukumbi wa matangazo ya matokeo huko katika hoteli ya Bwawani mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar – ZEC – KHATIB MWINYICHANDE amesema


FUONI
Waliojiandikisha 10884
Waliopiga kura 9367 %86.1
Kura halali 9201 %98.2
Zilizoharibika 166 %1.8
DK SHEIN CCM 6351 %69.0
Maalim Seif CUF 2777 %30.2
Kasim Bakr Ali wa jaahazi asilia ni 9 % 0.1


MTONI
Waliojiandikisha 9672
Waliopiga kura 8768 %90.7
Kura halali 8635 %98.5
Zilizoharibika 133 %1.5
DK SHEIN CCM 3746 %43.4
Maalim Seif CUF 4852 %56.2


DOLE

Waliojiandikisha 8017
Waliopiga kura 4912
Kura halali 6834 %98.4
Zilizoharibika 108% 1.6
DK SHEIN CCM 4777 %69.9
Maalim Seif CUF 2007 %6.4
Kasim Bakar wa jahazi asilia 16 % 0.1

DIMANI
Waliojiandikisha 12813
Waliopiga kura 11383 %88.8
Kura halali 11298 %68.5
Zilizoharibika 175 % 1.5
dk SHEIN 6225 % 55.5
Maalim Seif CUF 4898
Tadea na Jahazi asilia wamefuata kw akufungana kwa kura 23



Kiembe samaki
Waliojiandikisha 4998
Waliopiga kura 3856 %35.4
Kura halali 3806
Zilizoharibika 50 % 1.3
DK SHEIN CCM 4338
Maalim Seif CUF 2812
NCCR mageuzi 10

Mwanakwerekwe

Waliojiandikisha 8062
Waliopiga kura 7253 %90.3
Kura halali 7178 % 98.4
Zilizoharibika 115 % 1.6
DK SHEIN CCM 4338 % 60.4 2812 % 39 .2 NRA 10 %0.1
Maalim Seif CUF



BUBUBU
Waliojiandikisha 9809
Waliopiga kura 8827
Kura halali 8606
Zilizoharibika 121
DK SHEIN CCM 4458 %51.8
Maalim Seif CUF 4119 % 47.9
Nra 12 % 0.1


MFENESINI
Waliojiandikisha 7242
Waliopiga kura 6203% 85.7
Kura halali 6038
Zilizoharibika 165
DK SHEIN CCM 3755 %62.2
Maalim Seif CUF 2246%37.2
AFP 11 %0.2




AMANI
Waliojiandikisha 7641
Waliopiga kura 6857%
Kura halali 6725
Zilizoharibika 112 %1.6
DK SHEIN CCM 4567 % 64.9
Maalim Seif CUF 2312 %34.4


Raha leo
Waliojiandikisha 7229
Waliopiga kura 6399 %88.5
Kura halali 6300 %88.5
Zilizoharibika 99 %1.5
DK SHEIN CCM 4043 %64.2

Maalim Seif CUF 2216 %35.2


KIKWAJUNI
Waliojiandikisha 7910
Waliopiga kura 6513 %82.3
Kura halali 6431%98.7
Zilizoharibika 82 % 1.3
DK SHEIN CCM 4534 %70.5
Maalim Seif CUF 1860 % 28.9



KWAHANI

Waliojiandikisha 7497
Waliopiga kura 6459%86.2
Kura halali 6398 %99.1
Zilizoharibika 61 %0.9
DK SHEIN CCM 4994%78.1
Maalim Seif CUF 1349 %21.1



MJI MKONGWE

Waliojiandikisha 7495
Waliopiga kura 6414 %85.6
Kura halali 6334 %98.8
Zilizoharibika 80 %1.2
DK SHEIN CCM 1589 %25.1
Maalim Seif CUF 4717 %74.5



Magogoni
Waliojiandikisha 10101
Waliopiga kura
Kura halali
Zilizoharibika
DK SHEIN CCM 3867 %44.1
Maalim Seif CUF 4867 %55.4



MPENDAE
Waliojiandikisha 9459
Waliopiga kura 8596 %90.9
Kura halali 8476
Zilizoharibika 120
DK SHEIN CCM 4870 %57.5
Maalim Seif CUF 3546 %41.8



DONGE

AFP KURA 9, CCM-6320=88.4, CUF 773=10.8, JAHAZI ASILIA 28=0.1, NCCR-MAGEUZI 5=01%, NRA 5=0.1%, TADEA 11=0.2%




UZINI

AFP 14=0.2%, CCM 7158=89.9%, CUF 731, JAHAZI 29=0.3%, NCCR-MAGEUZI 7=0.1, NRA 8=0.1%, TADEA 12=0.2

CHWAKA

CCM 7365 81%

CUF 1610 17.7%

MUYUNI

CCM 6052 81%

CUF 1316 17.7%

KOANI

CCM 7247 69.3%

CUF 3099 29.7%

MAKUNDUCHI

CCM 6544 83%

CUF 1256 15%

MGOMBEA WA URAIS WA ZANZIBAR ANAONGOZA KATIKA MAJIMBO 12 YA MJINI MAGHARIBI

Chama cha mapinduzi CCM kinaongoza katika kura za urais wa Zanzibar kwenye majimbo 12 kati ya 15 ya mkoa wa mjini magharibi, huku chama cha wananchi CUF kikiongoza katika majimbo matano ya wilaya ya Wete.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Khatib Mwinyichande amesema mgombea wa CCM Dr. Ali Mohammed Shein ameshinda katika majimbo ya Fuoni, Dole, Dimani, Kiembesamaki, Mwanakwerekwe, Bububu, Mfenesini na Mpendae.

Majimbo mengine aliyoshinda Dr. Shein ni Amani, Rahaleo, Kikwajuni na Kwahani wakati mgombea wa CUF Seif Sharif Hamad ameshinda katika majimbo ya Mtoni, Magogoni na Mji Mkongwe.

Wagombea wengine wa vyama vya AFP, TADEA, NCCR-MAGEUZI, NRA, JAHAZI ASILIA na TADEA wamepata kura chini ya asilimia mbili katika majimbo hayo.

Na huko kisiwani Pemba mwandishi wetu alioko katika afisi ya uchaguzi wilaya ya Wete amesema kwa mujibu wa matokeo yaliotolewa na afisi hiyo kwa majimbo ya Kojani, Wete, Konde, Gando na Mtambwe, mgombea wa CUF Hamad anaongoza katika majimbo hayo…

Tume ya uchaguzi Zanzibar imesitisha kwa muda kutangaza matokeo ya urais wa Zanzibar katika majimbo yaliobakia hadi saa 3.00 asubuhi hii, lakini matokeo ya uwakilishi na udiwani yameanza kutangazwa katika afisi za uchaguzi za wilaya.

Uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa mfumo wa vyama vingi kwa mara ya kwanza umefanyika kwa amani na utulivu ikilinganishwa na chaguzi tatu zilizopita.