I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, November 1, 2010

DR SHENI ASHINDA KITI CHA URAIS ZANZIBAR

HAYAA WADAU MUDA MFUPI TUU TAYARI MATOKEO YA KURA ZA UCHAGUZI ZNZ ZIMEKWISHA KAMILIKA . MUDA MFUPI TU TUME IMEMTANGAZA DR SHENI KUWA NDIE ALIYE SHINDA KITI CHA URAIS ZNZ

HABARI KAMILI INAKUJA SOON

WAKATI WOWOTE KUTOKA SASA TUTAPATA KUMJUA RAIS MPYA WA ZNZ

Umati mkubwa wananchi umekusanyika mbele ya kituo cha kutangazia matokeo ya uchaguzi katika hoteli ya Bwawani wakiisindikiza tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika juzi yatolewe haraka badala ya kutangazwa kwa utaratibu wa kusuasua.

Wananchi hao walijaa ndani ya hoteli na ukumbi wa salama wa hoteli hiyo huku baadhi yao wakiwa nje ya geti ambapo jeshi la polisi lililazimika kufunga lango na kuwazuwia baadhi yao wasiingie ndani kutokana na kuwa ndani ya hoteli hiyo kulijaa umati mkubwa wa watu .

Vijana na akina mama walikuwa wengi katika lango la hoteli hilo huku wakiimba na nyimbo huzuni na kusoma quran tukufu na kumshitakia Mwneyenzi Mungu kwa kuomba dua za kumhifadhi Maalim Seif na balaa na kuitakia kheri Zanzibar na watu wake katika kipindi hiki cha utangazaji wa matokeo.

Jeshi la polisi jana lilionekana likifanya kazi kubwa na kuhakikisha usalama unapatikana katika eneo lote la hoteli hiyo ikiwa pamoja na kuwasogeza wafuasi hao wakiwataka wakae chini huku magari ya maji ya kemikali na polisi waliovalia kivita wakiwa pembeni kwa wafuasi hao.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wamesema hawataandoka maeneo hayo hadi hapo tume ya uchaguzi itakapotangaza matokeo ya urais kwani imekuwa ukichelewesha kwa makusudi na kuishutumu tume hiyo kwamba inataka kubadilisha matokeo halisi yaliokusanywa vituoni.

“Hapa hatutaondoka mpaka tusikie rais akitajwa maana huu ni uchaguzi wane unafanyika nchini kwetu lakini imekuwa kawaida kukawilishwa matokeo lakini sisi tunachotaka ni kutangazwa kwa matokeo na sio jambo jengine” alisema Asha Abdallah ambaye ni miongoni mwa akina mama waliokuja na watoto wake.

Wananchi hao ambao wengi wao wanaonekana ni wafuasi wa chama cha wananchi (CUF) wamesema wasingependa kufanya fujo wala kusababisha madhara kwa mwengine lakini kwa kuwa wanataka maoni yao yaheshimiwe hawana budi kutetea haki yao ambayo imekuwa ikiporwa kwa muda mrefu na watawala.

“Mtatusamehe sana waandishi wa habari na waangalizi sisi tumekuja hapa sio lengo letu kufanya fujo lakini lengo letu ni kuwa mawazo yetu na maamuzi yetu tulioamua ndani ya kisanduku cha kura tunataka yaheshimiwe na watawala kwa hivyo tunataka ushindi wa maalim seif apewe mwenyewe haraka..tunachotaka maalim seif atangazwe maana matokeo yanaonesha yeye anaongoza akifuatiwa na Dk Shein” alisema Hassan Hamad Nassor.

Tokea juzi tume ya uchaguzi Zanzibar kupitia mwenyekiti wake, Khatib Mwinyichande imekuwa ikitoa matokeo ya urais huku matokeo ya uwakilishi, udiwani na ubunge yakitolewa majimboni.

Kwa mujibu wa Khatib hadi sasa CUF imepata majimbo matatu kwa upande wa Unguja ikiwemo jimbo la Mji Mkongwe, Magogoni na Mtoni huku majimbo mengine mengi yaliotangazwa yakishikiliza na CCM ikiwemo la Donge na Uzini ambayo yameshinda kwa zaidi ya asilimia 90

WAGOMBEA UWAKILISHI NA UBUNGE KUTOKA CUF WAMESHINDA MAJIMBO YA PEMBA

Wagombea wa nafasi za uwakilishi na ubunge Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF wanaendelea kushinda katika majimbo mbali mbali kisiwani Pemba.

Matokeo ya hivi karibuni mgombea uwakilishi jimbo la Tumbe kwa tiketi ya CUF Rufai Said Rufai ameshinda jimbo hilo kwa kupata kura elfu tano 312 na kumshinda mpinzani wake wa karibu wa CCM Amour Khamis Mbarouk aliepata kura 470.

Matokeo ya ubunge jimbo la Mkoani Ali Khamis Seif wa CUF ameshinda jimbo hilo, jimbo la Mkanyageni Mohamed Habib Mnyaa wa CUF ameshinda jimbo la Mtambile mgomea wa CUF Masoud Abdala Salum ameshina ubunge jimbo hilo.

Jimbo la Kiwani mgombea ubunge wa CUF Abdala Haji Ali meshanda wa jimbo hilo, jimbo la Chambani mbunge ni Salum Hemed Khamis wa CUF. Mwandishi wetu Haji Nassoro kutoka Pemba

Na huko jimbo la Wawi mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CUF Hamad Rashid Mohame ameshinda kwa kupata kura elfu tano 321 na kumshinda mpinzani wake karibu kutoka CCM Daud Khamis Juma aliepata kura elfu mbili 255

KAZI ZA KUHESABU KURA ZA RAIS WA TANZANIA ZINAENDELEA KUHESABIA

Kazi za kuhesabu kura kwa ajili uchaguzi wa urais wa jamhuri ya muungano Tanzania zinaendelea katika maeneo mbali mbali hasa yale ya Tanzania bara.

Hata hivyo baadhi ya maeneo ya Zanzibar kazi za kuhesabu kura zimalizika na kinachosubiriwa ni kutangazwa kwa matokeo ya jumla ya tume ya taifa ya uchaguzi NEC.

Waangalizi wa kimataifa wamesema kazi za upigaji kura zilifanyika kwa amani na utulivu licha ya kujitokeza kasoro ndogo ndogo.

Mkurugenzi wa tume ya taifa ya uchaguzi NEC Rajab Kiravu amesema uchaguzi wa majimbo yakiwemo majimbo manne ya Zanzibar umeahirishwa kutokana na upungufu wa karatasi za kupigia kura.

Amesema uchaguzi huo utarejewa tena Novemba 14 mwaka huu

MATOKEO YA URAIS MAJIMBO YA PEMBA

ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.

WAWI
CCM 2024 25.0%,
CUF 6,036 74.4%,
AFP 13 0.2%,
JAHAZI ASILIA 11 0.1%,
NCCR MAGEUZI 12 0.1%,
NRA 7 0.1%,
TADEA 6 0.1%.

CHONGA
CCM 2,150 34.1%,
CUF 4,108 65.2%,
AFP 10 0.2%,
JAHAZI ASILIA 16 0.3%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%,
NRA 6 0.1%,
TADEA 3 0.0%.

OLE
CCM 8,93 13.7%,
CUF 5,775 86.2%,
AFP 6 0.1%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 4 0.1%,
NRA 6 0.1%,
TADEA 5 0.1%.

CHAKE
CHAKE CCM 1,575 21.9%,
CUF 5,530 77.7%,
AFP 12 0.2%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 2 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

MTAMBWE
CCM 307 5.4%,
CUF 5,415 74.4%,
AFP 1 0.0%, JAHAZI
ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 2 0.0%,
NRA 3 0.1%,
TADEA 4 0.1%.

KONDE
CCM 6,53 10.1%,
CUF 5,751 89.9%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 10 0.1%,
NCCR MAGEUZI 10 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

MTAMBILE
CCM 961 16.1%,
CUF 4,9818 83.5%,
AFP 3 0.1%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 5 0.1%,
TADEA 6 0.1%.

WETE
CCM 1,159 25.5%,
CUF 6,317 83.3%,
AFP 1 0.0%, JAHAZI
ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%, NRA 2 0.0%, TADEA 2 0.0%.

KOJANI
CCM 562 8.2%,
CUF 6,262 91.5%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 3 0.0%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 1 0.0%.

GANDO
CCM 8,84 14.4%,
CUF 5,239 85.4%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 8 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

MGOGONI
CCM 615 9.8%,
CUF 5,614 89.1%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 12.0%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 3 0.0%,
TADEA 0 0.0%.


ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.

ZIWANI
CCM 921 13.5%,
CUF 5,901 86.3%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 5 0.1%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 4 0.1%,
TADEA 1 0.0%.


KONDE CCM 6,53 10.1%,
CUF 5,751 89.9%,
AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 10 0.1%,
NCCR MAGEUZI 10 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 4 0.1%.

WETE CCM 1,159 25.5%,
CUF 6,317 83.3%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 6 0.1%,
NCCR MAGEUZI 8 0.1%,
NRA 2 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

KOJANI CCM 562 8.2%,
CUF 6,262 91.5%,
AFP 2 0.0%,
JAHAZI ASILIA 13 0.2%,
NCCR MAGEUZI 3 0.0%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 1 0.0%.

GANDO CCM 8,84 14.4%,
CUF 5,239 85.4%,
AFP 1 0.0%,
JAHAZI ASILIA 8 0.1%,
NCCR MAGEUZI 3 0.1%,
NRA 1 0.0%,
TADEA 2 0.0%.

MGOGONI CCM 615 9.8%,
CUF 5,614 89.1%, AFP 5 0.1%,
JAHAZI ASILIA 12.0%,
NCCR MAGEUZI 5 0.1%,
NRA 3 0.0%,
TADEA 0 0.0%

MATOKEO YA URAIS MAJIMBO 22 YA UNGUJA

TUME ya uchaguzi Zanzibar imetangaza matokeo ya awali ya nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa majimbo 18 ya Unguja na mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha mapinduzi CCM DK ALI MOHAMED SHEIN ameonekana kung,aa zaidi kwa ushindi wa majimbo mengi kisiwani Humo.
Akisoma matokeo hayo mbele ya waandishi wa habari,waalikwa,waangalizi wa uchaguzi na wananchi katika ukumbi wa matangazo ya matokeo huko katika hoteli ya Bwawani mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar – ZEC – KHATIB MWINYICHANDE amesema


FUONI
Waliojiandikisha 10884
Waliopiga kura 9367 %86.1
Kura halali 9201 %98.2
Zilizoharibika 166 %1.8
DK SHEIN CCM 6351 %69.0
Maalim Seif CUF 2777 %30.2
Kasim Bakr Ali wa jaahazi asilia ni 9 % 0.1


MTONI
Waliojiandikisha 9672
Waliopiga kura 8768 %90.7
Kura halali 8635 %98.5
Zilizoharibika 133 %1.5
DK SHEIN CCM 3746 %43.4
Maalim Seif CUF 4852 %56.2


DOLE

Waliojiandikisha 8017
Waliopiga kura 4912
Kura halali 6834 %98.4
Zilizoharibika 108% 1.6
DK SHEIN CCM 4777 %69.9
Maalim Seif CUF 2007 %6.4
Kasim Bakar wa jahazi asilia 16 % 0.1

DIMANI
Waliojiandikisha 12813
Waliopiga kura 11383 %88.8
Kura halali 11298 %68.5
Zilizoharibika 175 % 1.5
dk SHEIN 6225 % 55.5
Maalim Seif CUF 4898
Tadea na Jahazi asilia wamefuata kw akufungana kwa kura 23



Kiembe samaki
Waliojiandikisha 4998
Waliopiga kura 3856 %35.4
Kura halali 3806
Zilizoharibika 50 % 1.3
DK SHEIN CCM 4338
Maalim Seif CUF 2812
NCCR mageuzi 10

Mwanakwerekwe

Waliojiandikisha 8062
Waliopiga kura 7253 %90.3
Kura halali 7178 % 98.4
Zilizoharibika 115 % 1.6
DK SHEIN CCM 4338 % 60.4 2812 % 39 .2 NRA 10 %0.1
Maalim Seif CUF



BUBUBU
Waliojiandikisha 9809
Waliopiga kura 8827
Kura halali 8606
Zilizoharibika 121
DK SHEIN CCM 4458 %51.8
Maalim Seif CUF 4119 % 47.9
Nra 12 % 0.1


MFENESINI
Waliojiandikisha 7242
Waliopiga kura 6203% 85.7
Kura halali 6038
Zilizoharibika 165
DK SHEIN CCM 3755 %62.2
Maalim Seif CUF 2246%37.2
AFP 11 %0.2




AMANI
Waliojiandikisha 7641
Waliopiga kura 6857%
Kura halali 6725
Zilizoharibika 112 %1.6
DK SHEIN CCM 4567 % 64.9
Maalim Seif CUF 2312 %34.4


Raha leo
Waliojiandikisha 7229
Waliopiga kura 6399 %88.5
Kura halali 6300 %88.5
Zilizoharibika 99 %1.5
DK SHEIN CCM 4043 %64.2

Maalim Seif CUF 2216 %35.2


KIKWAJUNI
Waliojiandikisha 7910
Waliopiga kura 6513 %82.3
Kura halali 6431%98.7
Zilizoharibika 82 % 1.3
DK SHEIN CCM 4534 %70.5
Maalim Seif CUF 1860 % 28.9



KWAHANI

Waliojiandikisha 7497
Waliopiga kura 6459%86.2
Kura halali 6398 %99.1
Zilizoharibika 61 %0.9
DK SHEIN CCM 4994%78.1
Maalim Seif CUF 1349 %21.1



MJI MKONGWE

Waliojiandikisha 7495
Waliopiga kura 6414 %85.6
Kura halali 6334 %98.8
Zilizoharibika 80 %1.2
DK SHEIN CCM 1589 %25.1
Maalim Seif CUF 4717 %74.5



Magogoni
Waliojiandikisha 10101
Waliopiga kura
Kura halali
Zilizoharibika
DK SHEIN CCM 3867 %44.1
Maalim Seif CUF 4867 %55.4



MPENDAE
Waliojiandikisha 9459
Waliopiga kura 8596 %90.9
Kura halali 8476
Zilizoharibika 120
DK SHEIN CCM 4870 %57.5
Maalim Seif CUF 3546 %41.8



DONGE

AFP KURA 9, CCM-6320=88.4, CUF 773=10.8, JAHAZI ASILIA 28=0.1, NCCR-MAGEUZI 5=01%, NRA 5=0.1%, TADEA 11=0.2%




UZINI

AFP 14=0.2%, CCM 7158=89.9%, CUF 731, JAHAZI 29=0.3%, NCCR-MAGEUZI 7=0.1, NRA 8=0.1%, TADEA 12=0.2

CHWAKA

CCM 7365 81%

CUF 1610 17.7%

MUYUNI

CCM 6052 81%

CUF 1316 17.7%

KOANI

CCM 7247 69.3%

CUF 3099 29.7%

MAKUNDUCHI

CCM 6544 83%

CUF 1256 15%

MGOMBEA WA URAIS WA ZANZIBAR ANAONGOZA KATIKA MAJIMBO 12 YA MJINI MAGHARIBI

Chama cha mapinduzi CCM kinaongoza katika kura za urais wa Zanzibar kwenye majimbo 12 kati ya 15 ya mkoa wa mjini magharibi, huku chama cha wananchi CUF kikiongoza katika majimbo matano ya wilaya ya Wete.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Khatib Mwinyichande amesema mgombea wa CCM Dr. Ali Mohammed Shein ameshinda katika majimbo ya Fuoni, Dole, Dimani, Kiembesamaki, Mwanakwerekwe, Bububu, Mfenesini na Mpendae.

Majimbo mengine aliyoshinda Dr. Shein ni Amani, Rahaleo, Kikwajuni na Kwahani wakati mgombea wa CUF Seif Sharif Hamad ameshinda katika majimbo ya Mtoni, Magogoni na Mji Mkongwe.

Wagombea wengine wa vyama vya AFP, TADEA, NCCR-MAGEUZI, NRA, JAHAZI ASILIA na TADEA wamepata kura chini ya asilimia mbili katika majimbo hayo.

Na huko kisiwani Pemba mwandishi wetu alioko katika afisi ya uchaguzi wilaya ya Wete amesema kwa mujibu wa matokeo yaliotolewa na afisi hiyo kwa majimbo ya Kojani, Wete, Konde, Gando na Mtambwe, mgombea wa CUF Hamad anaongoza katika majimbo hayo…

Tume ya uchaguzi Zanzibar imesitisha kwa muda kutangaza matokeo ya urais wa Zanzibar katika majimbo yaliobakia hadi saa 3.00 asubuhi hii, lakini matokeo ya uwakilishi na udiwani yameanza kutangazwa katika afisi za uchaguzi za wilaya.

Uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa mfumo wa vyama vingi kwa mara ya kwanza umefanyika kwa amani na utulivu ikilinganishwa na chaguzi tatu zilizopita.

Sunday, October 31, 2010

WADAU TAYARI MATOKEO YA ZNZ YASHAANZA KUTOKA

WADAU MATOKEO TAYARI TUMEYAPA USIKU NA ASUHUHI HII MATOKEO YA PEMBA NA ZNZ.. MPAKA SASA NI MATOKEO YA URAIS TU NDIO YALIYOTOKA. KITAKWIM HADI SASA MAALIM SEIF ANAONGOZA KWA 74,603 TUKIJUMLISHA NA MAJIMBO YA PEMBA TULIYOYAPOKEAA. DR SHEIN ANA 68,493.. KWA PEMBA NA ZNZ. HADI SASA CCN HAIJASHINDA HATA JIMBO MOJA PEMBA KATIKA MAJIMBO YALIYO TANGAZWA. CUF IMESHINDA MAJIMBO MAWILI KATIKA MAJIMBO YALIYO TANZAZWA ZNZ. JIMBO LA MJI MKONGWE NA JIMBO LA MTONI. KWA SASA TUME IMESITISHA UTOWAJI WA MATOKEO HADI SAA 3 ASUBUHI..

WADAU MIMI NAENDA KULALA SIJUI NTAAMKA SAA NGAPI MAANA JANA NIKIKESHA .

BAADAE NTAWALETEA INFO .....

BADO TUNASUBIRI MATOKEO HADI SASA TUME HAIJATANGAZA KITU

Wadau mimi sasa nipo studio ndai Zenjifm hakuna kulala . Hapa nasubiri kuungana na wenzangu walioko bwawani ili kuwaletea matokeo moja kwa moja . so stay tune.... yakitoka tu na kwenye blog ntaweka . ntarud tena na info baada ya nusu saa.

UCHAGUZI WA ZANZIBAR 2010

Tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC imesema inatarajia kutangaza Matokeo mara baada ya kupokea Majumuisho ya Fomu zilizosainiwa na Mawakala kwa Majimbo mbali mbali ya Zanzibar.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC Salum Kassim Ali amesema hadi sasa hawajapokea Fomu yeyote ya Majumuisho licha ya kwamba Matokeo ya awali kubandikwa katika Vituo mbali mbali vya uchaguzi.
Amesema kitu ambacho kimejitokeza ni Mawakala vyama katika Majimbo kutosaini Fomu husika za Uchaguzi. Leo ndio uchaguzi umefanyika nchi nzima licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo zilizosababisha baadhi ya majimbo maa 4 ya unguja na pemba ya ubunge na wadi tisa kwa Zanzibar kutofanyika kutokana na hitilafu za karatasi za kupigia kura

TANGAZO LA TUME KWA WAANDISHI LATOKA SASA

HAYA JAMANII MUDA MFUPI TUU KUTOKA SASA MKUU WA TUME AMETANGAZA KUWA HADI SASA BADO HAJAPATA MATOKEO HATA YA JIMBO MOJA. NA KWA MUJIBU WA MKUU ANASEMA MAWAKALA WA VYMA NDIO WANAZOROTESHA KUPATIKANA KWA MATOKEO KWANI WAMEKUWA WAGUMU KUTIA SAIN KATIKA KUKUBALI MATOKEO ..... MATOKEO YAKITOKA TU UTAYAPATA HAPA LEO HAKUNA KULALA

MATOKEO YA UCHAGUZI ZANZIBAR 2010

STAY TUNE MUDA WOWOTE KUTOKA SASA NTAWEKA HEWANI

TUME YA UCHAGUZI TANZANIA IMEAHIRISHA UCHAGUZI WA MAJIMBO MANNE YA ZANZIBAR

Tume ya taifa ya uchaguzi NEC katika wilaya ya magharibi imeahirisha uchaguzi wa wabunge katika majimbo matatu ya wilaya ya magharibi kwa muda usiojulikana.

Akizungumza na Zenji Fm radio msimamizi wa uchaguzi NEC wilaya ya magharib Amina Talib Ali ameyataja majimbo hayo ni Magogoni, Mtoni na Mwanakwerekwe.

Amesema kuahirishwa kwa uchaguzi huo kunatokana na upungufu wa karatasi za kupigia kura zilizopokelewa kwa wagombea hao na kutaja upungufu huo ni wa kibinadamu…

Hata hivyo Amina amewataka wapiga kura katika majimbo hayo kutovunjika moyo na kuwataka kuzitunza shahada za kupigia kura hadi pale itakapotangazwa tarehe nyingine ya kufanyika uchaguzi huo.

Wakati huo huo tume ya uchaguzi ya taifa NEC imeahirisha uchaguzi katika jimbo la Wete kutokana na jina la mgombea ubunge wa chama cha TLP kutoonekana katika karatasi ya kupigia kura.

Hata hivyo kazi za upigaji kura katika mkoa wa Kaskazini Pemba zimendelea vizuri licha ya kujitokeza matatizo katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.

Katika jimbo la Ole kumejitokeza upungufu wa karatasi za kupigia kura kwa wabunge na rais wa jamhuri ya muungano Tanzania hali iliyosababisha kuchelewa kuanza kwa upigaji kura.

ZANZIBAR YAFANYA UCHAGUZI KWA AMANI NA UTULIVU

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania umeanza vizuri, licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo zilizosababisha baadhi ya majimbo ya matatu ya ubunge na wadi tisa kwa Zanzibar kutofanyika kutokana na hitilafu za karatasi za kupigia kura. Miongoni mwa wadi zilizoahirishwa uchaguzi huo ni Kajengwa, Mangapwani, Mchangani, Kwahani Miembeni, Nyerere na wadi tatu za Pemba na majimbo yaliohirishwa uchaguzi ni Mtoni, Mwanakwerekwe na Magogoni. Mwandishi wetu alietembelea vituo vya kupigia kura Mwanakwerekwe amesema baadhi ya mawakala wamelalamikia uhaba wa vitabu vya kupigia vya urais wa jamhuri ya muungano. Wakala wa CUF katika kituo cha Mwanakwerekwe amesema vitabu vilivyotarajiwa kuwepo katika vituo hivyo ni vitano, lakini vimefika vitatu hivyo kuna uwezekano kwa watu wengine kukosa kupiga kura. Akizungumzia suala hilo mkurugenzi wa tume ya uchaguzi Tanzania Rajab Kiravu amesema tayari makamishna wa tume hiyo wanafuatilia matatizo hayo katika vituo vya Tanzania bara na Zanzibar…

Nae mgombe mwenza wa chama cha ATPP-MAENDELEO Rashid Mchenga amesema iwapo baadhi ya wananchi watakosa kupiga kura kutokana na uchache wa vitabu uchaguzi utarejewe kulingana na sheria Hata hivyo akizungumza na Zenji Fm radio amesema uchaguzi umefanyika kwa amani na utulivu na kuwataka wagombea kukubali matokeo kwa maslahi ya taifa lao…

Na huko Tanzania bara baadhi ya wapiga kura mjini Dar es Salaam walilalamika tatizo la kutokuwemo kwa majina yao katika orodha ya wapiga kura. Kazi za kuhesabu kura zinatarajiwa kuanza katika vituo vyote vya kupigia kura na matokeo yake yatabandikwa katika vituo hivyo

UCHAGUZI WA ZANZIBAR 2010

TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR IMEAHIRISHA UCHAGUZI KATIKA WADI NNE ZA MKOA WA MJINI MAGHARIBI

Tume ya uchaguzi Zanzibar imeahirisha uchaguzi wa madiwani katika wadi nne za mkoa wa mjini magharibi kutokana na kukosewa kwa uchapishaji wa karatasi za kupigia kura kwa wagombea hao.

Akizungumza na waandishi wa habari huko hoteli ya Bwawani mkurugenzi wa tume hiyo Salum Kassim Ali amezitaja wadi hizo ni Mchangani jimbo la Mji mkongwe, Kwahani jimbo la Kwahani, Miembeni jimbo la Kikwajuni na wadi ya Nyerere jimbo la Magomeni.

Amesema hali hiyo inatokana na baadhi ya majina ya wagombea kuonekana katika wadi ambazo hawahusiki kupigiwa kura na baadhi ya wapiga kura kulazimika kupiga kura wadi sio zao.

Hata hivyo mkurugenzi huyo amesema uchaguzi wa madiwani katika wadi hizo utafanyika Jumapili ijayo tarehe 28 mwezi ujao na hakutakuwa na kampeni wala uteuzi wa wagombea.

Wakati huo huo Ali amesema vifaa vya kupigia kura zikiwemo karatasi za kupigia kura tayari vimeshasambazwa katika vituo vyote vya kupigia kura vya Unguja na Pemba vipatavyo elfu moja, 291.

Uchaguzi mkuu wa nne wa Zanzibar wa mfumo wa vyama vingi unatarajiwa kufanyika kesho ambapo jumla ya wapiga kura laki nne elfu saba, 658 watapiga kura kuwachagua wagomea urais wa Zanzibar, muungano, wawakilishi, wabunge na madiwani.

UCHAGUZI MKUU TANZANIA

Wananchi wa Tanzania wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa rais, bunge, uwakilishi na udiwani Jumapili ya tarehe 31 Octoba mwaka 2010.

Uchaguzi huo wa nne wa vyama vingi vya siasa kwa upande wa Zanzibar unaonekana kuwa na mchuano mkali kati ya mgombea wa urais wa CCM Dr. Ali Mohammed Shein na mgombea wa CUF Seif Sharif Hamad.

Jumla ya wapiga kura laki nne, elfu saba, 658 kwa upande wa Zanzibar watapiga kura kuwachagua wagombea urais wa jamhuri ya muungano Tanzania, urais wa Zanzibar, wabunge, wawakilishi na madiwani katika vituo vya kupigia kura vipatavyo elfu moja, 291 Unguja na Pemba.

Na huko Tanzania bara wapiga kura watawachagua wagomea urais wa jamhuri ya muungano, wabunge na madiwani. Kampeni za uchaguzi huo mkuu zinatarajiwa kumalizika rasmi hapo kesho

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetenga zaidi ya shilingi bilioni 2.5 kugharamia uchaguzi mkuu wa Zanzibar.

MAALIM SEIF AHIDI KUKUBALI MATOKEO YA UCHAGUZI

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF Seif Sharif Hamad amesema yuko tayari kukubali matokeo ya uchaguzi na kuwataka wafuasi wa chama hicho kutiofanya vurugu wakati wa kutangazwa matokeo hayo.

Hata hivyo mgombea huyo ametoa wito kwa tume ya uchaguzi Zanzibar kuendesha uchaguzi wa haki na huru na kuwasimamia maafisa wake wa wilaya ambao wanatiliwa shaka ya kutaka kuchafua uchaguzi.

Akizungumza katika mkutano wa mwisho wa kampeni za uchaguzi huko viwanja vya Maisara Maalim Seif amesema wakati umefika kwa wazanzibar kuachana na siasa za chuki na kuanza kutafuta njia za kujiiinua kimaendeleo.

Amesema wazanzibar wana kila sababu ya kuendeleza maridhiano ya kisiasa yanayolenga kuijenga Zanzibar mpya

Kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa itakayoundwa baada ya uchaguzi amesema endapo ataingia madarakani atahakikisha serikali hiyo inawajumuisha wazanzibari wote bila kujali udini na ukabila.

Amesema ataingoza Zanzibar kwa kutumia utawala wa sheria na hakuna kiongozi hata mmoja atakaekuwa juu ya sheria ili kuona kila mwananchi anapata haki yake.

Aidha mgombea huyo amesema endapo wananchi watamchagua serikali yake itaimarisha uchumu kwa asilimia 15 utakaolenga kuinua maisha ya wananchi kwa kuongeza nafasi za ajira.

RAIS KIKWETE KUONDOA SUALA LA MAFUTA KWENYE MUUNGANO

Mgombea urais wa Jamhuri ya muungano Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dr. Jakaya Kikwete ameahidi kulipatia ufumbuzi tatizo la uchimbaji wa mafuta ya Zanzibar katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Amesema matatizo mengi yaliodaiwa kuwa kero ya muungano tayari yameshapitiwa ufumbuzi, kupitia kamati ya pamoja ya waziri mkuu na waziri kiongozi na maeneo yaliobakia ikiwemo suala la uchimbaji wa mafuta ya Zanzibar kuondolewa katika muungano litapatiwa jawabu…

Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari ambapo Zenji Fm radio imetangaza moja kwa moja rais Kikwete pia ameahidi kuimarisha sekta ya uwekezaji ili kulipatia ufumbuzi tatizo la ajira.

Amesema tatizo la ajira kwa vijana bado ni kubwa nchini, lakini amesema endapo atachaguliwa tena kuiongoza Tanzania serikali yake itawavutia wawakezaji kwa kuwawekea mazingira mazuri.

Rais Kikwete amesema mpango huo utakwenda sambamba na kuwawezesha wakezaji wazalendo kwa kuwapatia mikopo ya kuwekeza katika viwanda, huduma na biashara ili kusaidia ukuwaji wa uchumi.

Aidha Dr. Kikwete amesema serikali yake itaanzisha benki ya wakulima na kuongeza fedha katika taasisi za fedha zinazotoa mikopo yenye masharti nafuu ili kuwawezesha wananchi kujiajiri na kuwajiri wengine…….)

Sunday, September 26, 2010

UCHAGUZI WA ZANZIBAR 2010

PROFISA LIPUMBA APATA AJALI TANGA

Msafara wa mgombea urais wa jamhuri ya muungano Tanzania kupitia chama cha wananchi CUF Profisa Ibrahim Harouna Lipumba umepata ajali leo asubuhi mkoani Tanga.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Handeni imehusisha magari mawili ya yaliokuwa katika kampeni, moja ilimbeba meneja wa kampeni na mgombea urais Profisa Lipumba na nyingine jingine limewabeba wandishi wanne wa habari.

Ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo la mgombea kuchomoka tairi na kupoteza mwelekeo. Hata hivyo mgombea huyo na meneja wa kampeni Saidi Miraj hawakupata majeraha, lakini walikimbizwa hospitali kwa ajili ya kuangaliwa afya zao.

Gari ya waandishi wa habari wanne ilipinduka mara mbili, lakinihakuna mwandishi hata mmoja aliepata majeraha makubwa

MUASISI WA MAPINDUZI ZANZIBAR SAID ABDALLA NATEPE AMEFARIKI DUNIA

Mmoja wa viongozi 14 wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar,Meja Jenerali Abdallah Said Natepe amefariki dunia jana mchana katika hospitali yajeshi Lugalo mjini Dar es Salaam.

Marehemu Natepe ni miongoni mwa viongozi wa mapinduzi kumbi na mbili waliofariki dunia ambao walifanikisha kufanikiwa kwa mapinduzi ya Januari 12, 1964 yaliyoindoa serikali ya kisultani visiwa vya Zanzibar,

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, kifo hicho kimetokea jana mchana kwenye hospitali hiyo kuu ya Jeshi la Wananchi.
Taarifa hiyo inamnukuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akieleza kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha mwanamapinduzi huyo na kumtumia salamu za rambirambi katibu mkuu wa CCM akielezea jinsi alivyoguswa na kifo hicho cha Mzee Natepe.

“Kifo kimemchukua mwanamapinduzi, mzalendo na mwanachama wetu mwaminifu katika kipindi ambacho taifa na chama bado kinamhitaji sana. Kifo kimetunyang’anya tunu wakati huu tunaoelekea uchaguzi mkuu; ni huzuni kubwa kwetu; ni majonzi makubwa na hatuna neno kubwa linaloweza kuelezea huzuni hii,” Rais Kikwete anakaririwa kwenye taarifa hiyo.

Rais alipokea taarifa za kifo cha Mzee Natepe jana mchana akiwa Njombe mkoani Iringa ambako yuko kwa ajili ya shughuli za kampeni.

Rais Kikwete pia ametuma salaamu za rambirambi kwa familia, ndugu na jamaa wa Marehemu Natepe.

“Mzee Natepe amekuwa sehemu ya maisha yangu ya kisiasa, kijamii na amenipa malezi na maelekezo mengi nikiwa kama kijana wake na amekuwa moja ya nguzo yangu kubwa katika shughuli zangu za kisiasa na kikazi katika maeneo yote niliyotumikia nchi yangu,” alisema rais na kuelezea kwa masikitiko huzuni aliyonayo na kuwahakikishia kuwa yuko nao katika kipindi hiki kigumu.

“Tunamshukuru mwenyezi Mungu kwa kutupa nafasi ya kuishi na Mzee Natepe na kufanya naye kazi. Tunamuomba Mungu amlaze mzee wetu mahali pema peponi na kumpa pumziko la milele, amina”

MGOMBEA WA CUF MALIM SEIF AHADI KUCHIMBA MAFUTA NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MITANO

Chama cha wananchi CUF kimesema endapo kitaingia madarakani kuingoza Zanzibar suala la mafuta na gesi asilia litaondolewa kwenye orodha ya mambo ya muungano ndani ya kipindi cha miaka mitano.

Mgombea urais kupitia chama hicho Malim Seif Sharif Hamad amesema suala la mafuta na gesi asilia kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya muungano halina lengo la kuvunja muungano bali ni kujali uchumi wa nchi ndogo na kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Ocean View mjini hapa amesema tayari baadhi ya makampuni yameonesha nia ya kutaka kuchimba mafuta yaliopo Zanzibar hivyo serikali yake itatakeleza suala hilo ndani ya kipindi cha miaka mitano.

DR. SHEIN AHIDI KUWARUDISHA MATAJIRI WAZALENDE KWENDA KUEKEZA PEMBA

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dr. Ali Mohammed Shein amesema serikali yake itaendelea kuimarisha miundo mbinu ya kiuchumi kisiwani Pemba ili kuwainua kiuchumi wananchi wa kisiwa hicho endapo atapata ridhaa ya kuiongoza Zanzibar.

Amesema wawekezaji kutoka nje ya nchi na wale wazalengo wanaokeza nchi za kigeni wameonesha nia ya kuja kuwekeza Zanzibar hasa maeneo ya Pemba kutokana na kuwepo vivutio vya kiuchumi kama vile umeme wa uhakika, maji na miundo mbunu ya usafirishaji.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho kisiwani Pemba Dr. Shein amesema endapo wananchi watamchagua serikali yake itaandaa sera maulum za kuendeleza uchumi kisiwani Pemba kupitia ilani ya uchaguzi.

Amefahamisha kuwa usalama, amani na utulivu wa wananchi utaisaidia Zanzibar kuendeleza sekta za uwekezaji kwa kuwashajihisha wawekezaji wazalendo wanaowekeza nchi za nje pamoja na wawekezaji wageni kuja kuwekeza nchini...

Kuhusu utumishi wa umma Dr. Sheina amesema endapo ataingia madarakani serikali yake itaangalia maslahi ya wafanyakazi kwa kuwapatia mafunzo ya muda mrefu na mfupi, nyenzo, na kuongeza na mslahi yao.

Amesema wafanyakazi ndio kiini cha mapinduzi ya Zanzibar, hivyo wanahitaji kuendelezwa kwa kupewa taaluma ya kuwatumikia wananchi kwa ufanisi badala ya kubahatisha ili kuliletea tija taifa lao.

Nae mgombea mwenza Dr. Mohammed Gharib amewataka wana CCM kisiwani Pemba kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu ili kuhakikisha chama hicho kinaleta ushindi kwa wagombea wake.

Wednesday, September 15, 2010

CUF YAZINDUA ILANI YAKE YA UCHAGUZI YA MWAKA 2010 ZANZIBAR

Chama cha wananchi CUF kimesema kitaangalia upya mambo yaliongezwa katika orodha ya mambo ya muungano baada ya makubaliano ya awali ya mwaka 1964 yaliounda muungano huo endapo kitapewa ridhaa ya kuongoza Zanzibar.

Mgombea wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Seif Sharif Hamad amesema mambo hayo yatajadiliwa kwa kina na uwazi ili kuhakikisha muungano huo unazifaidisha nchi zote mbili kwa msingi ya usawa.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010 ya chama hicho amesema serikali yake pia itawasiliana na serikali ya muungano kutaka kuandika katiba mpya itakayokidhi makubaliano ya muungano ya mwaka 1964 yenye muundo wa serikali tatu

Kuhusu maendeleo ya uchumi Hamad amesema serikali atakayoiunda itajenga uchumi imara kwa kuzingatia mfumo wa soko huria unatoa fursa ya ushiriki wa wananchi wote ili kuona hali zao za kimaisha zinaimarika.

Amesema sekta za kilimo, utalii, biashara, viwanda na uvuvi zitapewa umuhimu katika ujenzi wa uchumi wa kisasa pamoja na kuhakikisha matumizi bora ya raslimali ziliopo ikiwemo uchimbaji wa mafuta.

Hamad amesema serikali yake itaanzisha shirika la ndege kwa njia ya ubia na wewekezaji wa ndani na nje ili kuwa na njia za uhakika za kuinganisha Zanzibar kibiashara na kiuchumi na nchi nyingine duniani.

Amesema atafanya mazungumzo na mashirika ya kimataifa ya usafiri wa anga kuanzisha usafiri wa moja kwa moja kati ya miji mikuu yao na Zanzibar ili kuimarisha shughuli kiuchumi na biashara…

Kuhusu utumishi wa umma Hamad amesema serikali yake itapandisha mishahara ili iweze kukidhi gharama za maisha na kuhakikisha inatolewa kila baada ya wiki mbili na ambapo kima cha chini kitaanzia shilingi laki moja na nusu.

Amesema licha ya serikali kuwa na wafanyakazi wengi wasiokuwa na tija serikalini, serikali yake itakuwa na mpango maalum wa mashauriano ya kutoa maamuzi baadhi ya wafanyakazi ambao hawana tija serikalini waondolewe.

Amesema wafanyakazi hao watejengewa mazingira mazuri ya kuwa na ajira mbadala ili kuweza kuzalisha au kutoa huduma zenye tija zitakazomuwezehsa kupata mapato makubwa kuliko alivyokuwa serikalini.

Friday, September 10, 2010

KATIBU MKUU WA CUF HAMAD AMSIFU RAIS KARUME KWA KUIACHA ZANZIBAR KUWA NA AMANI

Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Seif Sharif Hamad, amesifu juhudi za rais wa Zanzibar Dr. Amani Abeid Karume, anaeondoka madarakani kwa kuiacha Zanzibar kuwa nchi ya amani.

Amesema busara za rais Karume katika kusimamia maridhiano ya kisiasa, zinahitaji kupongezwa kwa vile zimesababisha kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa, mara baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba 31 mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kumaliza sherehe za baraza la Edil fitr huko Forodhani, Hamad pia amesifu maendeleo ya kiuchumi yaliofikiwa na serikali ya rais Karume, katika ujenzi wa miundo mbinu ya kiuchumi na kijamii…

Kuhusu uendeshaji wa kampeni za kisiasa kwa ajili ya uchaguzi mkuu, katibu mkuu huyo amewataka viongozi wenzake wa kisiasa kuendesha kampeni za kistaarabu, ili kuenzi umoja na mshikamno wa wazanzibari uliopo.

RAIS KARUME AMEWATAKA VIONGOZI WA SIASA KUENDESHA KAMPENI ZA KISTAARABU

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid Karume, amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuendesha kampeni za uchaguzi mkuu kwa kuheshimiana, umoja, amani na utulivu.

Amesema siasa sio ugomvi bali ni sehemu ya kutekeleza mahitaji ya watu, hivyo ni vyema kwa wananchi na viongozi wa siasa kuimarisha hali ya utulivu, ili kulinda maridhianoya kisiasa yalioleta umoja na mshikamano.

Akilihutubia baraza la Ediel fitr huko Forodhani, rais Karume amesema katika kipindi kilichopita cha utulivu wa kisiasa nchini, kimeleta mafanikio ya uchumi na ustawi wa jamii, kama vile ujenzi wa miradi ya miundo mbinu, elimu, afya, sekta za huduma na utalii

Hata hivyo rais Karume anaemaliza muda wake, baada ya kufanyika uchaguzi mkuu Octoba 31, amesema juhudi zaidi zinahitajika kuendeleza nyanja nyingine za maendeleo kwa faida ya kila mwananchi.

Amesema wananchi hawanabudi kujituma zaidi, ili kuona mipango ya serikali, kama vile mkakati wa kukuza uchumi na kuondoa umasikini MKUZA na malengo ya Milenia inafanikiwa kwa lengo la kuinua pato la taifa.

Baraza hilo la edil fitr, linalofanyika baada ya waislamu kumaliza wamwezi mtukufu wa ramadhan, pia limehudhuriwa na viongozi wa vyama vya siasa na mabalozi wadogo wanaoziwakilisha nchi zao Zanzibar.

ZANZIBAR KUTARAJIWA KUKUBWA NA UKAME

Baadhi ya maeneo ya Unguja na Pemba yanatarajiwa kukumbwa na ukame utakaosababisha uhaba wa malisho na maji kwa ajili ya mifugo na kilimo cha umwagiliaji maji kutokana uhaba wa mvua za vuli zinazotarajiwa kuanza wiki ya pili mwezi ujao.

Taarifa ya mamlaka ya hali hewa Tanzania iliyotolewa kwa vyombo vya habari imesema hali hiyo inatokana na mvua za vuli kunyesha chini ya kiwango kitakacho athiri unyevunyevu wa kuotesha miti, mazao na malisho ya mifugo.

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania imewashauri wakulima na wafugaji kutumia maji kwa uangalifu, kuotesha mazao yanayostahamili ukame na kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo katika maeneo yao.

Akizungumza na Zenji Fm Radio juu ya taarifa hiyo inayotishia kuathiri mifugo na kilimo cha umwagiliaji maji hapa Zanzibar mkurugenzi wa mamlaka ya hali ya hewa Zanzibar Khamis Ali Suleiman amesema

Taarifa hiyo ya hali ya hewa inayoashiria uhaba wa mvua za vuli imetolewa na wataalmu wa hali ya hewa wa nchi za eneo la Pembe ya mashariki mwa Afrika waliokutana mjini Nairobi Kenya kuanzia Agost 23 hadi Septemba tatu mwaka.

HOTELI NNE ZA KITALII ZANZIBAR ZIMEWAKA MOTO

Hoteli nne za kitalii na nyumba 12 za wananchi katika kijiji cha Nungwi Mkoa wa Kusini Unguja zimeteketea kwa moto leo mchana.

Katika tukio hilo hakuna mtu aliejeruhiwa, huku baadhi ya mali zilizokuwemo ndani ya hoteli hizo zimeripotiwa kuteketea kwa moto na nyingine zimewahi kutolewa na wasamaria wema.

Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo wamesema awali waliona moto na moshi mkubwa ukitokea katika maeneo yenye hoteli za kitalii na baadae moto huo kusambaa katika hoteli nyengine ambazo zilikuwa zikiwaka kwa kasi kubwa kutokana na upepo uliokuwa ukivuma baharini nyakti hizo.

Wamesema kikosi cha zima moto na ukozi kilichelewa kufika katika eneo la tukio, huku likiwa halina maji na kulazimika kutumia maji ya bahari lakini baadae lilikwama na kusababishwa moto huo kuchelewa kuzimwa. Hata hivyo mkuu wa Zima moto Sajenti Shukuru amesema wamemaliza kuzima moto huo na kukanusha madai kwamba gari lilikuwa halina maji na kukwama ufukweni

Kamanda wa ppoli mkoa wa kuskazini Unguja, Mselem Masoud Mtulya alithibitisha kutokea kwa moto huo na kuzitaja hoteli zilizoungua ni pamoja na Rummi ambayo imeteketea vibaya sana kwa kuwa ndio iliyoanza kuwaka na baadae moto huo kusambaa na kurukia katika hoteli iitwayo Bwagamoyo ambayo imeungua paa lote la hoteli hiyo.

Kamanda Mtulya alisema baadae moto huo ulishika katika hoteli ya Union ambayo nayo imeungua vibaya vyumba vya kulala na eneo lote la baa, ukumbi wa chakula na maduka ya vifaa na nguo za kitalii yaliokuwa ndani ya hoteli hiyo.

Aliitaja hoteli nyengine ni Diving Center ambayo nayo ilitekeleta katika eneo lake la ukumbi uitwao East Afrcan, ukumbi wa jambo brothers, sehemu ya jikoni yote imeungua na baadhi ya vyumba na kumbi zake zikiwa zimetekeleata vibaya sana.

Aidha alisema licha ya moto huo kusambaa kwa kasi lakini wageni wanane waliokuwa wamelala ndani waliwahi kuokolewa huku wengine wakiwa wamekimbia ambao wengi wao nyakati hizo walikuwa nje ya hoteli hizo na baadhi yao walikuwa wakipunga upepo na wengine walikuwa katika sehemu za kulia wakijipatia chakula.

Alisema nyumba za wananchi nazo hazikusalimika kutokana na moto huo ambapo zaidi ya nyumba 12 ambazo zipo karibu ya hoteli hizo zilizoungua zimeshika moto kutokana na moto huo kusambaa kwa kasi kutokana na upepo na kuwa zimeezekwa paa za makuti ambazo hushika moto haraka.

Kamanda Mtulya alisema chanzo cha moto huo hakijajulikana bado lakini jeshi la polisi linajitahidi kutafuta chanzo halisi cha kuzuka moto huo kabla ya kutoa taarifa sahihi kwa vyombo vinavyohusika.

Hasara iliyoptaikana kutokana na moto huo bado haijajulikana. Hii ni mara ya pili kwa hoteli za kitalii kuungua moto kwa kipindi kisichozidi miezi miwili ambapo tukio la mwanzo hoteli tatu kwa pamoja ziliungua moto katika kijiji cha Bwejuu Mkoa wa Kusini Unguja.

Tatizo la hoteli kuungua moto limekuwa likitokea mara kwa mara visiwani Zanzibar ambapo mwezi uliopita jumla ya hoteli za kitalii na nyumba zaidi ya sita ziliteketea kwa moto katika kijiji cha Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.

Hoteli zilizoungua mwezi uliopita ni pamoja na Visitors Inn, Sau Inn na Bungalow ambapo zote zipo eneo la Jambiani ukanda wa pwani ambapo kumbi na zaidi ya vyumba 12 vya kulala wageni viliteketea kutokana na moto huo.

Monday, September 6, 2010

MWENYEKITI WA TLP AGUSTINE LYATONGA ADAI KUFANYIWA RAFU KATIKA KAMPENI ZA UCHAGUZI

Mgombea ubunge jimbo la Vunjo ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour TLP, Agustine Mrema, amenusurika kujeruhiwa na kundi la vijana aliodai wafuasi wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Akizungumza na Zenji Fm radio Mrema amesema mbali ya kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe na vioo vyote vya mbele vya gari yake vimepasuliwa.

Amesema tukio hilo, limetokea Jumamosi iliyopita katika eneo la njia panda la Himo, Moshi wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura

WAANGALIZI WA UCHAGUZI WAMEANZA KUSAMBAZWA KUANGALIA UCHAGUZI MKUU 2010

Kamati ya kuangalia mwenendo wa uchaguzi Tanzania TEMCO imesema inashindwa kutekeleza shughuli za uangalizi wa chaguzi zinazofanyika nchini kutokana na uhaba wa fedha.

Mratibu wa TEMCO DR. Benson Banner amesema taasisi hiyo inayofanya kazi muhimu, lakini haipokei fungu lolote la fedha kutoka serikalini na badala yake hutegemea wahisani wenye masharti magumu.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari wa utowaji wa taarifa ya mwenendo wa uchaguzi mwaka 2010 mjini Zanzibar amesema hali hiyo imeifanya TEMCO kuwa na wangalizi wachache ikilinganishwa na ukubwa wa maeneo ya uchaguzi Tanzania.

Dr. Banner amesema taasisi za ndani zina uwezo mkubwa wa kuendesha shughuli za uangalizi wa chaguzi zinazofanyika nchini ikilinganishwa na taasisi za kimataifa, lakini bado haiziwezeshwi kifedha na serikali

Nae makamo mwenyekiti wa tume hiyo Maryam Abdulrahman amesema TEMCO inatarajia kutuma wangalizi wa uchaguzi elfu saba, 210 katika majimbo yote ya Tanzania bara na Zanzibar kuangalia mwenendo wa uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba mwaka huu.

Amesema wangalizi hao wa muda mrefu na mfupi watatumwa majimboni na kwenye vituo vya kupigia kura kuangalia undeshaji wa kampeni, upigaji na kuhesabu kura, utowaji wa matokeo, malalamiko na ukataji wa rufaa ambapo taarifa zake zitatolewa ndani ya siku tano baada ya upigaji wa kura.

TEMCO ni taasisi ya ndani inayoundwa na taasisi mia moja na 52 imekuwa ikiangalia mwenendo wa uchaguzi Tanzania tokea mwaka 1995.

BIDHAA MBOVU ZIMEZAGAA ZANZIBAR

Bidhaa zilizopitwa na viwango zimeanza kuzagaa katika kipindi hichi cha kumalizia mwezi mtukufu wa ramadhani ambazo huuzwa kwa bei nafuu.

Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari kutokana na uingizaji wa bidhaa mbovu ulioshamiri hapa Zanzibar hasa kipindi hiki cha kukaribia siku kuu ya Edil fitr.

Hatua hiyo imekuja kufuatiwa kuwepo kwa wimbi kubwa la uingizaji wa vyakula vilivyopita na muda wa matumizi ya binadamu ambalo limezuwa malalamiko kutoka kwa wananchi

Uchunguzi uliofanywa na Zenji Fm radio leo na jana umegundua mchele mbovu aina ya Busmat wenye ujazo wa kilo tano ukiuzwa kwa shilingi elfu sita na tano katika maeneo ya Darajani mjini Zanzibar.

Mchele huo unaouzwa na wafanyabiashara za mikononi maarufu wamachinga unaonesha kutengenezwa March 2008 na kumaliza muda wa matumizi March 2011 ni mbovu na unatoa harufu mbaya unapofunguliwa.

Akizungumza na zenji Fm radio juu ya malalamiko hayo mrajisi wa bodi ya chakula, dawa na vipodozi Dr. Burhan Simai amesema bodi hiyo haina sheria ya kuwadhibiti wafanyabiashara wanaojulikana wamachinga.

Hata hivyo amesema bodi hiyo inafanya ukaguzi katika sehemu zote zinazoingizwa bidhaa Unguja na Pemba na kukagua makontena yote ya bidhaa

Hivi karibuni hiyo imekamata tani 245 za mtama na tani 193 za mchele kutoka nje ya nchi zikiwa zimeharibika na havifai kwa matumizi ya binadamu.

Kutokana na hali hio Dk Simai aliwataka wananchi kuchukua tahadhari wakati wanaponunu

ZANZIBAR YAJENGA MATUMAINI KUPATA UANACHAMA WA FIFA

Naibu waziri kiongozi Ali Juma Shamhuna amesema juhudi za Zanzibar kupatiwa uwanachama wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA zimeanza kuleta matumaini baada ya kufunguliwa jalada rasmi la kuomba uanachama huo.

Shamhuna ambae pia ni waziri wa habari, utamaduni na michezo amesema rais wa FIFA Seif Blata ameahidi kulishughulikia ombi la Zanzibar la kupatiwa uwanachama wa shirikisho hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar wakati akitokea Uswiss Shamhuna amezitaja baadhi ya hoja zilizowasilishwa kuomba uanachama huo ni kuwepo nchi ndogo nandi ya FIFA ambazo hadhi zake zinazidiwa na Zanzibar, huku zikiwa sio wanachama wa umoja wa mataifa.

Mwaka 2001 Zanzibar ilishindwa kupata uwanachama wa shirikisho hilo na mwaka huu ilianda hoja nzito za kuomba uanachama huo ambazo zinamwelekeo wa kuzaa matunda.

Sunday, September 5, 2010

CHAMA CHA NLD, ZANZIBAR KUMUUNGA MKONO MGOMBEA WA URAIS ZANZIBAR KUPITIA CCM DR. ALI SHEIN

Chama cha siasa cha NLD, kimekuwa chama cha kwanza cha upinzani kutangaza kumuunga mkono mgombea wa urais wa Zanzibar kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dr. Ali Mohammed Shein katika uchaguzi mkuu ujao. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, naibu katibu mkuu wa NLD, Zanzibar Rashid Ahmme Joy amesema chama hicho kimeamuwa kumuunga mkono mgombea huyo kutokana na sera zake zenye kulenga siasa za umoja na kuweka mbele maslahi ya Zanzibar. Amesema chama hicho bado kina wasiwasi na wagombea wengine wa vyama vya kwamba hawatoweza kuendeleza siasa za umoja kwa kile alichodai kuwa na ulafi wa madaraka… “Sisi tutamuunga mkono mgombea atakaeleta mabadiliko na wagombea wa vyama vya upinzani watakapokuja hujui watafanya nini, hivyo mgombea wa CCM Dr. Shein ameonesha mwelekeo wa kufuata sera za siasa za umoja wa nchi”. Alisema Joy. Joy ambae kwa muda wa miezi kadhaa hajaonekana hadharani kutokana na kuugua shindikizo la damu amesema hali yake inaendelea vizuri na wiki mbili zijazo anatarajia kushiriki katika harakati za siasa. Hivyo amewaahidi wafuasi na wapenzi wa chama cha NLD ataendelea kuwepo katika ulingo wa kisiasa kwa lengo la kuleta mabadiliko ya mfumo wa siasa wa vyama vingi hasa Zanzibar. Chama cha NLD hakijasimamisha mgombea wa nafasi ya urais Zanzibar kutokana na Joy alietarajiwa kugombea nafasi hiyo kuugua siku chache baada ya tume ya uchaguzi Zanzibar kuanza kazi za utowaji wa fomu kwa wagombea wa nafasi hiyo kupitia vyama vya siasa. Hivi karibuni chama kingine cha upinzani cha APPT-MAENDELEO kimetangaza kumuunga mkono mgombea wa urais wa Zanzibar kupitia chama cha wananachi CUF Seif Sharif Hamad. END

Friday, September 3, 2010

BENKI YA WATU WA ZANZIBAR KUIMARISHA HUDUMA ZAKE

Benki ya watu wa Zanzibar PBZ, inakusudia kuweka mitandao itayowawezesha wateja wake wa ndani na nje ya nchi kupata huduma za kuweka, kutoa na kupokea fedha popote walipo.

Kaimu mkurugenzi wa PBZ Bw. Ame Haji Makame amesema hayo katika hafla futari iliyoandaliwa na benki hiyo huko hoteli ya Zanzibar Beach Rasort nje kidogo ya Zanzibar na kuhudhuriwa na rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid Karume na wateja wengine wa PBZ.

Amesema uwekezaji huo unahusisha uwekaji wa mashine za ATM, mtandao utakaowaruhusu wateja kutoa na kuchukua fedha katika matawi yote ya PBZ na mtandao wa kimataifa wa kutuma na kupokea fedha kwa njia ya haraka kutoka nje ya Tanzania.

Amesema PBZ pia inaendelea na ujenzi wa tawi la benki kwa ajili ya wateja wakubwa katika eneo la Mlandege mjini Zanzibar ambalo linatarajiwa kumalizika baada ya miezi mitatu na ujenzi wa tawi jingine mjini Dar es Salaam unaotarajiwa kumalizika mwezi Novemba.

Aidha Bw. Haji ameitaja miradi mingine itakayoiwezesha PBZ kumudu soko la ushindani ni ujenzi wa tawi la Chakechake Pemba pamoja na kujiunga na mfumo wa kutuma na kupokea fedha wa Western Union.

Amesema mfumo huo utasaidia serikali katika upokeaji wa fedha kati ya Zanzibar na nchi nyingine duniani na unatarajiwa kumalizika baada ya miezi miwili

RAIS KARUME ATEMBELEA UJENZI WA BARA BARA KISIWANI PEMBA

AIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk. Amani Abeid Karume ametoa pongezi kwa Idara ya Barabara Pemba pamoja na wananchi wa Mtambile,Kangani, Kengeja na Mwambe kwa kushiriki vyema katika ujenzi wa barabara zinazopita vijijini mwao.

Rais Karume alitoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa katika ziara ya kutembelea ujenzi wa barabara za Mtambile-Kangani na barabara ya Mtambile,Kengeja-Mwambe Kisiwani Pemba.

Katika ziara yake hiyo Rais Karume alitoa pongezi kwa wananchi wa maeneo hayo ambao wamekuwa wakishiriki kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa barabara ikiwa ni miongoni mwa barabara zilizomo kwenye Mradi wa Barara za vijijini Kusini Pemba.

Rais Karume aliwataka wananchi wa maeneo hayo kuongeza juhudi zaidi katika shughuli hiyo ya ujenzi wa brabara ambapo wananchi hupata ajira kwa kiasi kikubwa kutegemea na juhudi zao za kazi.

“Shukrani kwa msaada na mchango wenu mkubwa katika ujenzi wa barabara hivyo ongezeni juhudi na nguvu ili mpate kuendelea na ujenzi kwa ufanisi mkubwa”,alisema Rais Karume.

Akitembelea ujenzi wa barabara hizo ambazo kwa asilimia kubnwa ujenzi wake umekuwa ukiwashirikisha wananchi wenyewe, Rais Karume alisifu juhudi za wananchi hao.

Nae Muhandisi Mkaazi wa Idara ya Barabara Pemba, Khamis Masoud alimueleza Rais Karume kuwa kazi zinaenda vizuri na kuna matumaini makubwa ya kumaliza kwa wakati na kwa ufanisi zaidi.

Masoud alisema kuwa barabara hizo ni miongoni mwa barabara 6 zenye urefu wa kilomita 44.7 ambazo zimo katika Mradi huo wa Barabara za vijijini Kusini Pemba.

Alisema kuwa kazi nyingi za mwanzo katika ujeni huo zimeshalkuwa tayari kwa upande wa barabara ya Mtambile-Mwambe yenye urefu wa kilomita 9.4 ambapo tayari kilomita 2 zimeshaaza kutiwa lami.

Aidha, Masoud alisema kuwa kwa upande wa barabara ya Mtambile-Kangani yenye urefu wa kilomita 6.4 nayo kazi zake za ujenzi zinaenda vizuri. Pia, alisema kuwa barabara ya Miingani-Wambaa yenye urefu wa kilomita 9.7 nayo imo kwenye mchakato mbapo baada ya hapo barabara ya Kenya-Chambaani itafuatia.

Katika maelezo yake Mhandisi Mkaazi huyo alieleza kuwa kutokana na wananchi wengi kupata mafunzo juu ya ujenzi wa barara hatua hiyo imeweza kurahisisha ujenzi huo wa barabara ambapo hufanya kazi kwa makundi baada ya kupata utaalamu.

Masoud alisema kuwa utaalamu unaotumika wa Emulsion Treated Base (ETB) katika ujenzi wa barabara hizo kisiwani Pemba ambao hutumia lami baridi ni ujenzi wa mwanzo kwa nchi za Afrika za Mashariki na tayari nchi mbalimbali zimeomba kuja kisiwani Pemba kupata mafunzo zikiwemo Kenya, Msumbiji na nyenginezo

Kwa mujibu wa maelezo ya Mhandisi huyo ujenzi wa barabara hizo sita zilizomo katika Mradi huo unatarajiwa kukamilika Disemba mwaka 2011.

Barabara hizo zinajengwa na Idara ya Barabara chini ya ufadhili wa Serikali ya Norway hadi kumalizika kwake zitatumia zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 9.

Nao wananchi wa vijiji hivyo wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti walisifu juhudi za Rais Karume katika kuimarisha Maendeleo na uchumi wa Zanzibar ikiwa ni pamoja na kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya barabara.

Walieleza kuwa juhudi za Rais Karume za kuimarisha miundombinu ya barabara kisiwani Pemba ni mkombozi mkubwa wa uchumi na maendeleo ya nchi na wananchi wake kwani faida kubwa itapatikana baada ya kumaliza ujenzi wa barabara hizo a,mbapo wananchi watarahisishiwa kufanya biashara kwa uhakika, kuimarisha kilimo, uwekezaji, uvuvi na shughuli nyengunezo.

Katika ziara yake hiyo, Rais Karume alifuatana na viongozi mbali mbali akiwemo Mkewe Mama Shadya Karume.

Jioni ya leo Rais Karume anatarajiwa kujumuika na Waislamu na Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa ajili ya futari ya pamoja aliyowaandalia huko katika viwanja vya Ikulu ndogo ChakeChake Pemba.

Wednesday, September 1, 2010

RAIA WA AFRIKA YA KUSINI AJINYONGA KISIWANI PEMBA

Raia mmoja wa Afrika ya kusini amekutwa amekufa baada ya kujinyonga chumbani kwake katika hoteli ya Manta Riff iliyopo Micheweni Kisiwani Pemba.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kaskazini Pemba Rashid Yahya Bugi amesema raia huyo alitambuliwa kwa jina la James Ignatus White mwenye umri wa miaka 21 ni mfanyakazi wa hotel ya Manta Riff.

Amesema jeshi la polisi mara baada ya kupokea taarifa za tukio hilo lilikwenda katika eneo hilo na kuukuta mwili wa White ukiwa ananinginia katika kamba aliyojitundika.

Hata hivyo amesema chanzo cha kujiua kwa raia huyo wa kigeni bado hakijafahamika kwa vile hajawacha ujumbe wowote…

Mwili wa marehemu umekabidhiwa kwa uongozi wa hoteli ya Manta Riff kwa ajili ya kuusafirisha nchini kwao Afrika ya Kusini.

MAELFU YA WAUMINI WA KISLAMU WAMZIKA MUFTI MKUU WA ZANZIBAR

Maelfu ya waumini wa dini ya kislamu na wananchi wengine leo wamehudhuria maziko ya mufti mkuu wa Zanzibar sheikh Harith bin Helf aliefariki nchini India Alhamis iliyopita.

Maziko hayo yaliofanyika kijijini kwao Muyuni Wilaya ya Kusini yameongozwa na makamo wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Ali Mohammed Shein.

Viongozi wengine waliohudhuria maziko hayo ni rais mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi, waziri kiongozi wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha na mufti mkuu wa Tanzania bara Sheikh Shaaban bin Simba na viongozi wengine wa serikali na kidini.

Marehemu Harith amezaliwa mwaka 1927 katika kijiji cha Muyuni alipata elimu ya msingi mwaka 1937 na elimu ya chuo kikuu cha Alzhar nchini Misri na kuchaguliwa mufti mkuu wa Zanzibar mwaka 1992.

Marehemu alifariki dunia nchini India katika hospitali ya Miyot alikukuwa akitibiwa ugonjwa wa moyo na uti wa mgongo. Mungu ailaze roho ya marehemu peponi amina.

CHADEMA YATAKA RAIS KIKWETE AWEKEWE PINGAMIZI

Chama cha Demokraisa na maendeleo CHADEMA kimewasilisha malalamiko kwa msajili wa vyama vya siasa kikitaka mgombea wa urais wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM rais Jakaya Kikwete awekewe pingamizi katika kinyanganyiro cha uchaguzi wa urais.

Hoja kuu ya CHADEMA kuweka pingamizi ni kwa serikali kupandisha mishahara ya wafanyakazi waliokusudia kugoma wakati wa mkutano wa uchumi wa dunia, lakini rais Kikwete wakati huo alisema hawezikupandisha mishahara.

Kaimu katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika amesema hatua ya sasa ya serikali kupandisha mishahara ya watumishi wa umma inahesabiwa kama yenye kutaka ungwaji mkono na wafanyakazi.

Mnyika amedai suala la nyongeza wa mishahara kwa wafanyakazi halikuongezwa na bunge kama vile ilivyopendekezwa hivyo suala hilo linatumiwa kama kampeni za mgombea huyo na kwenda kinyume na sherria ya gharama za uchaguzi

MGOMBEA URAIS KUPITIA SAU ASHINDWA KUREJESHA FOMU

Ikiwa leo ni siku ya mwisho kurejesha fomu za kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar, mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama Cha Sauti ya Umma (SAU) Haji Mussa Kitole ameshindwa kurejesha fomu za kuwania nafasi hiyo kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Kitole awali alikataliwa kupewa fomu ya kuwania nafasi hiyo na ZEC kutokana na kuwa chama hicho kimetoa wagombea urais wawili wenye kutaka kuwania urais wa Zanzibar wakati sheria za ZEC zinaeleza chama kitowe mgombea mmoja wa nafasi hiyo.

Vyama ambavyo vimerejesha fomu leo katika afisi hiyo ni NCCR-MAGEUZI, TADEA, AFP, NRA, Jahazi Asilia huku chama cha SAU kikiwa bado hakijarejesha fomu hiyo.

Akizungumza na Zenji fm radio afisa wa habari wa tume ya uchaguzi Zanzibar Idriss Haji Jecha amesema hadi kufikia saa 9.45 cha cha SAU bado hakijarejesha fomu ambapo muda wa mwisho ulikuwa saa 10.00 jioni.

Amesema katika urejeshaji wa fomu hizo hakukuwa na kasoro zozote na fomu zilizorejeshwa zilikuwa safi.

SAU ndio chama pekee kilichoshindwa kuwasilisha fomu zake kwa tume ya uchaguzi ambapo vyama vyengine vilivyorejesha fomu zake jana ni pamoja Juma Ali Khatib (46) -TADEA, saa 4:13 asubuhi, Said Soud Said (62) AFP,saa 5:00, Haji Ambar Khamis (44) NCCR–Mageuzi, saa 5:30, Kassim Bakari Ali (43) Jahazi Asilia, saa 7.06, na Haji Khamis Haji (60) NRA saa 8:20 mchana.

Wengine waliorejesha fomu zao kwa ZEC wa mwanzo ni ni Mgombea wa chama cha wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ((67) alirejesha Agosti 16 majira ya saa 9:00 mchana wakati mgombea wa chama cha mapinduzi (CCM) Dk Ali Mohammed Shein (62) alijesha fomu yake Agosti 18 majira ya saa 8:30 mchana.

Akizungumza katika kikao hicho baada ya kupokea fomu hizo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Khatib Mwinchande alisema kwao wao kujitokeza kwa wagombea wengi ni kupanuka kwa demokrasia nchini.

Mwenyekiti huyo aliwaomba wagombea wote ambao watateuliwa na tume kuingia katika mchakato wa kutaka urais baada ya kuhakikiwa fomu zao kuingia katika kampeni za kistaarabu zisizo na matusi ili kuepusha Zanzibar kuingia katika sura mbaya ya kukosekana amani.

Iwapo wagombea urais kutoka vyama hivyo hawatawekewa pingamizi uchaguzi mkuu kwa nafasi ya urais unatarajiwa kufanyika Octoba 31 mwaka huu utakuwa na wagombea saba

MGOMBEA URAIS KUPITIA SAU ASHINDWA KUREJESHA FOMU

Ikiwa leo ni siku ya mwisho kurejesha fomu za kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar, mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama Cha Sauti ya Umma (SAU) Haji Mussa Kitole ameshindwa kurejesha fomu za kuwania nafasi hiyo kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Kitole awali alikataliwa kupewa fomu ya kuwania nafasi hiyo na ZEC kutokana na kuwa chama hicho kimetoa wagombea urais wawili wenye kutaka kuwania urais wa Zanzibar wakati sheria za ZEC zinaeleza chama kitowe mgombea mmoja wa nafasi hiyo.

Vyama ambavyo vimerejesha fomu leo katika afisi hiyo ni NCCR-MAGEUZI, TADEA, AFP, NRA, Jahazi Asilia huku chama cha SAU kikiwa bado hakijarejesha fomu hiyo.

Akizungumza na Zenji fm radio afisa wa habari wa tume ya uchaguzi Zanzibar Idriss Haji Jecha amesema hadi kufikia saa 9.45 cha cha SAU bado hakijarejesha fomu ambapo muda wa mwisho ulikuwa saa 10.00 jioni.

Amesema katika urejeshaji wa fomu hizo hakukuwa na kasoro zozote na fomu zilizorejeshwa zilikuwa safi.

SAU ndio chama pekee kilichoshindwa kuwasilisha fomu zake kwa tume ya uchaguzi ambapo vyama vyengine vilivyorejesha fomu zake jana ni pamoja Juma Ali Khatib (46) -TADEA, saa 4:13 asubuhi, Said Soud Said (62) AFP,saa 5:00, Haji Ambar Khamis (44) NCCR–Mageuzi, saa 5:30, Kassim Bakari Ali (43) Jahazi Asilia, saa 7.06, na Haji Khamis Haji (60) NRA saa 8:20 mchana.

Wengine waliorejesha fomu zao kwa ZEC wa mwanzo ni ni Mgombea wa chama cha wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ((67) alirejesha Agosti 16 majira ya saa 9:00 mchana wakati mgombea wa chama cha mapinduzi (CCM) Dk Ali Mohammed Shein (62) alijesha fomu yake Agosti 18 majira ya saa 8:30 mchana.

Akizungumza katika kikao hicho baada ya kupokea fomu hizo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Khatib Mwinchande alisema kwao wao kujitokeza kwa wagombea wengi ni kupanuka kwa demokrasia nchini.

Mwenyekiti huyo aliwaomba wagombea wote ambao watateuliwa na tume kuingia katika mchakato wa kutaka urais baada ya kuhakikiwa fomu zao kuingia katika kampeni za kistaarabu zisizo na matusi ili kuepusha Zanzibar kuingia katika sura mbaya ya kukosekana amani.

Iwapo wagombea urais kutoka vyama hivyo hawatawekewa pingamizi uchaguzi mkuu kwa nafasi ya urais unatarajiwa kufanyika Octoba 31 mwaka huu utakuwa na wagombea saba

TATIZO LA SOMALIA NI UINGILIAJI KATI WA MATAIFA YA KIGENI-HIZB UT-TAHARIR

Jumuiya ya kislamu ya kimataifa ya Hiz Ut-Tahrir imepinga ungiliaji kati unaofanywa na mataifa ya kigeni katika mzozo unaoendelea nchini Somalia kati ya wanamgambo wa Al-shabab na serikali ya mpito ya nchi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa naibu mwakilishi wa wa vyombo vya habari vya Jumuiya hiyo Afrika Mashariki Massoud Mselem amesema mzozo wa Somalia hauhitaji nguvu za kijeshi bali ni kuangalia kiini cha tatizo lenyewe.

Amesema suluhisho la amani ya Somalia sio kupambana na wanamgambo wa Al-Shabab bali ni kupinga uingiliaji kati wa masuala ya nchi hiyo dhidi ya mataifa ya kigeni…

Akizungumzia mateso na vitendo viovu wanavyofanyiwa waislamu wa Tajikistan Masoud ameitahadharisha dola hiyo na kusema iwapo hasara itatokea itarejea upande wa taifa hilo na kusema chama hicho kitajitolea kulingania utukufu wa mwezi mungu.

Amesema serikali ya Tajikistan inafanya makosa hayo huku ikiungwa mkono na madola ya magharibi na taasisi zinazodai kutetea haki za binadamu zikiwa zimekaa kimya.

Masoud amefahamisha zaidi ya waislamu 300 wa Tajikistan wanaendelea kusulubiwa kwa mateso, uonevu na vifungo vya muda mrefu.

Amesema Hiz ut-Tahrir Afrika Mashariki inalaani mateso na uharamia wanaofanyiwa waislamu wasiokuwa na hatia na utawala wa nchi hiyo unaongozwa na rais Rahmanov.

Jumuiya ya Hiz ut-Tahrir ni chama cha kislamu cha kimataifa chenye malengo ya kurejesha tena uislamu kupitia dola ya Helaf iliyoangushwa mwaka 1924.

RAIS KARUME AFUNGUA NYUMA YA WATOTO YATIMA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akifungua pazia kama ishara ya Uzinduzi wa Nyumba mpya ya watoto Yatima iliyopo Mazizini nje ya Mji wa Zanzibar

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr. Amani Abeid Karume amewataka wazazi na walezi kuchukuwa tahadhari ya kutowachia watoto wao kudhubaa mitaani.

Akifungua nyumba mpya ya kulelea watoto huko Mazizini nje kidogo ya mji wa Zanzibar mesema tabia hiyo itawajenga watoto kuishi maisha ya taabu na yasiokuwa na malengo yao ya baadae.

Dr. Karume amesema serikali ya Mapinduzi Zanzibar haiwezi kuiachia hali hiyo ikitokea kwa vile wazanzibari wote ni familia moja na wanadhamana ya kuwalea watoto wote.

Amesema mara baada ya mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 rais wa kwanza Abeid Karume ameanzisha kituo cha kulelea watoto huko Forodhani ili kuona watoto hao wanalelewa katika mazingira mazuri…

Aidha Dr. Karume amesema serikali imeamuwa kuwahamisha watoto wanaolelewa katika kutuo cha Forodhani kutokana na mazingira yaliopo katika eneo hilo hayafai tena kulelea watoto.

Amesema jengo hilo la Forodhani litaendelea kuwa mali ya serikali na kutumika kwa shughuli za makumbusho ya usafiri wa bahari ya Hindi chini ya usimamizi wa taasisi ya Agakhan Foundation.

Akizungumza katika ufunguzi wa kituo hicho katibu wa afisi ya Mufti mkuu Zanzibar Sheikh Fadhili Soraga amewataka waislamu kuendelea kuwatunza watoto yatima kulingana na mafundisho ya dini yao.

Amesema watu wanaowadhulumu watoto yatima kwa kula mali zao ni kwenda kinyume na mafundisho ya dini ya kislamu na watu hao tayari wameshabashiriwa kuingia motoni

Nyumba hiyo mpya ya kulelea watoto yenye ghorofa moja, vyumba vya kuishi watoto 80 kwa wakati mmoja, ukumbi wa mikutano, vyumba vya kompyuta, kusomea, na zahanati ujenzi wake umesimamiwa na taasisi ya ZAYADESA na kugharimu zaidi ya shilingi milioni 883

MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR KUPITIA CCM DR. SHEIN AREJESHA FOMU

Mgombea wa urais Zanzibar kupitia CCM Dr. Ali Mohammed Shein amesema ataitumikia Zanzibar kwa ufanisi mkubwa na kuweka mbele maslahi ya wananchi.

Akizungumza na wana CCM huko Kisiwandui muda mfupi baada kurudisha fomu za kuwania nafasi hiyo katika tume ya uchaguzi Zanzibar amesema atashirikiana vizuri na viongozi watakaokubali kufanyakazi kwa maslahi ya Zanzibar.

Aidha Dr. Shein ameonya kuwa hatamvumilia kiongozi yoyote ambae atakwenda kinyume na matakwa ya Wazanzibar endapo ataingia madarakani ……

Dr. Shein amesema katika uchaguzi ujao, CCM imejiandaa kuendesha kampeni za kistaarabu zenye kuwaelekeza wananchi malengo ya chama hicho ili wakipe ridhaa tena ya kuiongoza Zanzibar.

Nae naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar Saleh Ramadhan Ferouz amewataka wafuasi wa chama hiho kupuuza matamshi yanayotolewa na baadhi ya watu kwamba kumtilia kura kiongozi wa upinzani ni sawa na kumpigia mgombea wa CCM.

Amesema watu hao wanaopotosha wana CCM kwa kusambaza vipeperushi vyenye ujumbe huo, amewataka wafuasi wa chama hicho kuwa makini juu ya mbinu hizo zinazofanywa na vyama vya upinzani.

Dk . Shein anakuwa mgombea wa pili kurejesha fomu zake kwa tume ya uchaguzi Zanzibar kati ya wagombea wanane waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 31 mwaka huu.

TANZANIA YATAKIWA KUBADILISHA KATIBA

Mgombea wa urais wa Jamhuri ya muungano Tanzania kupitia chama cha wananchi CUF Profia Ibrahim Harouna Lipumba amesema wakati umefika kwa watanzania kurekebisha katiba ili kuruhusu mgombea binafsi na kupanua wigo wa demokrasia nchini.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni wa chama hicho kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mjini Dar es Salaam Profisa Lipumba amesema kutokuwepo kwa fursa hiyo kunanyima mianya ya demokrasia na kuwacha watu wenye sifa za kuongoza kutokana na kutojiunga na vyama vya siasa.

Aidha Profisa Lipumba amesema endapo atachaguliwa kuwa rais amesema atapunguza umasikini unaowakabili watanzania……

Hii ni mara ya nne kwa profisa Lipumba kuwania urais wa Jamhuri ya muungano Tanzania kupita CUF tangu mfumo wa vyama vingi kuanza mwaka 1992.

CHADEMA KUMUWEKEA PINGAMIZI RAIS KIKWETE

Kaimu katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA John Mnyika amesema chama hicho kinaendelea na taratibu zake katika afisi ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi ya taifa kupinga kile alichodai mgombea wa urais kupitia CCM rais Jakaya Kikwete kukiuka sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010.

` Wakati CHADEMA ikiendelea na harakati hizo naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania Bara Peuce Msekwa amesema mgombea huyo hajavunja kifungu chochote cha sheria na inasubiri suala hilo liwasilishwe katika afisi husika ili itowe utetezi wake.

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa mgombea urais wa wa CHADEMA Dr. Wilbord Slaa amepanga kuwasilisha pingamizi kwa msajili wa vyama vya sisasa nchini John Tendwa kwa madai mgombea urais wa CCM rais Jakaya Kikwete amevunja kifungu nambari 21 cha sehria ya gharama za uchaguzi.

MUFTI MKUU WA ZANZIBAR AFARIKI DUNIA NCHINI INDIA

Mufti mkuu wa Zanzibar Sheikh Harith bin Khelef Khamis amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nchini India katika hospital ya Meyot ambapo alikuwa anapata matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mufti imesema kwamba Mufti amefariki dunia jana asuhuhi katika hospitali ya Meyot Mjini Chanay nchini Idia

Katibu wa Mufti Sheikh Fadhil Suleiman Soraga amesema Zanzibar imepata msiba mkubwa kwa kuondokewa na kiongozi wake huku akisisitiza wananchi kuwa na subra katika msiba huo.

“Nchi yetu imepatwa na msiba mkubwa sana kwa kuondokewa na kiongozi mkuu wa dini visiwani ambaye alikuwa matibabuni kwenye hospitali ya Meyot Mjini Chenay nchini India” alisema Sheikh Soraga.

Soraga alisema mipango ya kusafirisha mwili wa mrehemu inaendelea kwa mashirikiano makubwa na ubalozi wa Tanzania nchini India huku maandalizi ya kuupokea mwili wa marehemu kwa heshima zote za kitaifa yanaendelea.

Alisema wananchi wataelezwa rasmi juu ya suala hilo lilipofikia baada ya kuwasili kwa maiti na muda wa mazishi hayo yatapangwa baada ya kufika Zanzibar mwili wa marehemu.

“Kwa taarifa hii waumini na wananchi wote kwa ujumla wanaombwa kuwa watulivu na kuungana pamoja katika kuukabili msiba huu mkubwa kitaifa” alisema taarifa hiyo iliyosainiwa na katibu wa Mufti Sheikh Soraga.

Licha ya kuwa taarifa ya serikali haikueleza Mufti alipelekwa nchini India kwa ugonjwa gani lakini taarifa za undani zinasema kwamba alipelekwa baada ya kuugua kwa muda mfupi akisumbuliwa na matatizo ya figo.

Akizungumza bila ya kutaka kutajwa jina lake gazetini kwa madai kwamba sio msemaji wa familia alisema wakati wa uhai wake Sheikh Harith alikataa kusafirishwa kupelekwa India kutokana na hali yake lakini baada ya kuonekana hali yake imezidi kuzorota ilimshauri kumpeleka matibabuni India.

Hatika hatua nyengine takriban misikiti yote leo Zanzibar imetoa tangazo la kifo cha Mufti na kuwataka waumini wamuombee dua katika kipindi hiki muhimu cha mwezi mtukufu wa ramadhani.

“Tuna masikitiko makubwa kwa kuondokewa na kiongozi wetu msomi wetu na muumini mwenzetu Mufti wa Zanzibar Sheikh Harith Bin Khelef huko nchini India alipokwenda kwa matibabu kwa hivyo tumuombeeni sana dua Mwenyeenzi Mungu amsameh madhambi yake” alisema Sheikh Abrahaman Habshi imamu mkuu wa msikiti wa Jibril Mkunazini.

Mufti Khelef mwenye umri wa miaka 80 ni miongoni mwa wasomi na wanazuoni wakubwa ambao wamebahatika kusoma katika chuo kikuu maarufu cha Kiislamu kiliopo Misri Al-Azhar katika miaka ya 1960.

Chuo kikuu cha Al-Azhar ni maarufu sana katika bara la Afrika na duniani ambacho hutoa elimu mbali mbali za dini ya kiislamu pamoja na masomo mengine ya lugha za kiarabu.

Marehemu Khelef aliteuliwa kuwa Mufti mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika mwaka 1995 wakati wa uongozi wa rais mstaafu Dk Salmin Amour Juma.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka India inafanywa na ofisi ya mufti wa Zanzibar ambayo ipo chini ya Wizara ya nchi Ofisi ya Rais Katiba na Utawala bora.

MUFTI MKUU WA ZANZIBAR AFARIKI DUNIA NCHINI INDIA

Mufti mkuu wa Zanzibar Sheikh Harith bin Khelef Khamis amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nchini India katika hospital ya Meyot ambapo alikuwa anapata matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mufti imesema kwamba Mufti amefariki dunia jana asuhuhi katika hospitali ya Meyot Mjini Chanay nchini Idia

Katibu wa Mufti Sheikh Fadhil Suleiman Soraga amesema Zanzibar imepata msiba mkubwa kwa kuondokewa na kiongozi wake huku akisisitiza wananchi kuwa na subra katika msiba huo.

“Nchi yetu imepatwa na msiba mkubwa sana kwa kuondokewa na kiongozi mkuu wa dini visiwani ambaye alikuwa matibabuni kwenye hospitali ya Meyot Mjini Chenay nchini India” alisema Sheikh Soraga.

Soraga alisema mipango ya kusafirisha mwili wa mrehemu inaendelea kwa mashirikiano makubwa na ubalozi wa Tanzania nchini India huku maandalizi ya kuupokea mwili wa marehemu kwa heshima zote za kitaifa yanaendelea.

Alisema wananchi wataelezwa rasmi juu ya suala hilo lilipofikia baada ya kuwasili kwa maiti na muda wa mazishi hayo yatapangwa baada ya kufika Zanzibar mwili wa marehemu.

“Kwa taarifa hii waumini na wananchi wote kwa ujumla wanaombwa kuwa watulivu na kuungana pamoja katika kuukabili msiba huu mkubwa kitaifa” alisema taarifa hiyo iliyosainiwa na katibu wa Mufti Sheikh Soraga.

Licha ya kuwa taarifa ya serikali haikueleza Mufti alipelekwa nchini India kwa ugonjwa gani lakini taarifa za undani zinasema kwamba alipelekwa baada ya kuugua kwa muda mfupi akisumbuliwa na matatizo ya figo.

Akizungumza bila ya kutaka kutajwa jina lake gazetini kwa madai kwamba sio msemaji wa familia alisema wakati wa uhai wake Sheikh Harith alikataa kusafirishwa kupelekwa India kutokana na hali yake lakini baada ya kuonekana hali yake imezidi kuzorota ilimshauri kumpeleka matibabuni India.

Hatika hatua nyengine takriban misikiti yote leo Zanzibar imetoa tangazo la kifo cha Mufti na kuwataka waumini wamuombee dua katika kipindi hiki muhimu cha mwezi mtukufu wa ramadhani.

“Tuna masikitiko makubwa kwa kuondokewa na kiongozi wetu msomi wetu na muumini mwenzetu Mufti wa Zanzibar Sheikh Harith Bin Khelef huko nchini India alipokwenda kwa matibabu kwa hivyo tumuombeeni sana dua Mwenyeenzi Mungu amsameh madhambi yake” alisema Sheikh Abrahaman Habshi imamu mkuu wa msikiti wa Jibril Mkunazini.

Mufti Khelef mwenye umri wa miaka 80 ni miongoni mwa wasomi na wanazuoni wakubwa ambao wamebahatika kusoma katika chuo kikuu maarufu cha Kiislamu kiliopo Misri Al-Azhar katika miaka ya 1960.

Chuo kikuu cha Al-Azhar ni maarufu sana katika bara la Afrika na duniani ambacho hutoa elimu mbali mbali za dini ya kiislamu pamoja na masomo mengine ya lugha za kiarabu.

Marehemu Khelef aliteuliwa kuwa Mufti mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika mwaka 1995 wakati wa uongozi wa rais mstaafu Dk Salmin Amour Juma.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka India inafanywa na ofisi ya mufti wa Zanzibar ambayo ipo chini ya Wizara ya nchi Ofisi ya Rais Katiba na Utawala bora.

MUFTI MKUU WA ZANZIBAR AFARIKI DUNIA NCHINI INDIA

Mufti mkuu wa Zanzibar Sheikh Harith bin Khelef Khamis amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nchini India katika hospital ya Meyot ambapo alikuwa anapata matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mufti imesema kwamba Mufti amefariki dunia jana asuhuhi katika hospitali ya Meyot Mjini Chanay nchini Idia

Katibu wa Mufti Sheikh Fadhil Suleiman Soraga amesema Zanzibar imepata msiba mkubwa kwa kuondokewa na kiongozi wake huku akisisitiza wananchi kuwa na subra katika msiba huo.

“Nchi yetu imepatwa na msiba mkubwa sana kwa kuondokewa na kiongozi mkuu wa dini visiwani ambaye alikuwa matibabuni kwenye hospitali ya Meyot Mjini Chenay nchini India” alisema Sheikh Soraga.

Soraga alisema mipango ya kusafirisha mwili wa mrehemu inaendelea kwa mashirikiano makubwa na ubalozi wa Tanzania nchini India huku maandalizi ya kuupokea mwili wa marehemu kwa heshima zote za kitaifa yanaendelea.

Alisema wananchi wataelezwa rasmi juu ya suala hilo lilipofikia baada ya kuwasili kwa maiti na muda wa mazishi hayo yatapangwa baada ya kufika Zanzibar mwili wa marehemu.

“Kwa taarifa hii waumini na wananchi wote kwa ujumla wanaombwa kuwa watulivu na kuungana pamoja katika kuukabili msiba huu mkubwa kitaifa” alisema taarifa hiyo iliyosainiwa na katibu wa Mufti Sheikh Soraga.

Licha ya kuwa taarifa ya serikali haikueleza Mufti alipelekwa nchini India kwa ugonjwa gani lakini taarifa za undani zinasema kwamba alipelekwa baada ya kuugua kwa muda mfupi akisumbuliwa na matatizo ya figo.

Akizungumza bila ya kutaka kutajwa jina lake gazetini kwa madai kwamba sio msemaji wa familia alisema wakati wa uhai wake Sheikh Harith alikataa kusafirishwa kupelekwa India kutokana na hali yake lakini baada ya kuonekana hali yake imezidi kuzorota ilimshauri kumpeleka matibabuni India.

Hatika hatua nyengine takriban misikiti yote leo Zanzibar imetoa tangazo la kifo cha Mufti na kuwataka waumini wamuombee dua katika kipindi hiki muhimu cha mwezi mtukufu wa ramadhani.

“Tuna masikitiko makubwa kwa kuondokewa na kiongozi wetu msomi wetu na muumini mwenzetu Mufti wa Zanzibar Sheikh Harith Bin Khelef huko nchini India alipokwenda kwa matibabu kwa hivyo tumuombeeni sana dua Mwenyeenzi Mungu amsameh madhambi yake” alisema Sheikh Abrahaman Habshi imamu mkuu wa msikiti wa Jibril Mkunazini.

Mufti Khelef mwenye umri wa miaka 80 ni miongoni mwa wasomi na wanazuoni wakubwa ambao wamebahatika kusoma katika chuo kikuu maarufu cha Kiislamu kiliopo Misri Al-Azhar katika miaka ya 1960.

Chuo kikuu cha Al-Azhar ni maarufu sana katika bara la Afrika na duniani ambacho hutoa elimu mbali mbali za dini ya kiislamu pamoja na masomo mengine ya lugha za kiarabu.

Marehemu Khelef aliteuliwa kuwa Mufti mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika mwaka 1995 wakati wa uongozi wa rais mstaafu Dk Salmin Amour Juma.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka India inafanywa na ofisi ya mufti wa Zanzibar ambayo ipo chini ya Wizara ya nchi Ofisi ya Rais Katiba na Utawala bora.

Thursday, August 5, 2010

UN YATOA PONGEZI KWA ZANZIBAR

UMOJA wa Mataifa umetoa pongezi zake kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume na wananchi wote wa Zanzibar kwa kufanikisha kura ya maoni kwa amani na utulivu.

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro aliyasema hayo wakati alipokuwa na mazungumzo na Rais Karume, Ikulu mjini Zanzibar.

Dk. Migiro, alimueleza Rais Karume kuwa Umoja wa Mtaifa umeridhika na hatua iliyofikiwa katika kufanikisha zoezi zima la kura ya maoni kwa amani, utulivu na mafanikio makubwa.

Akitoa salamu za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-moon, Dk. Migiro alieleza kuwa, UN imeridhishwa na makubaliano yaliyofanyika kati ya Rais Karume kupitia chama cha CCM na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kwa lengo la kuondosha kabisa migogoro iliyokuwepo hapo kabla.

Katika salamu hizo, Ban Ki-moon aliwatakia kila la heri wananchi wa Zanzibar katika kujenga amani na umoja ambao utawasaidia katika kufikia lengo lililokusudiwa ambapo UN itaendelea kutoa ushirikiano wake ili kuweza kupata mafanikio zaidi.

Katibu Mkuu huyo wa UN, aliipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuweza kusimamia vyema zoezi hilo kwa salama na amani.

Aidha, Dk. Migiro alimueleza Rais Karume kuwa UN imefarajika kwa namna Serikali anayoiongoza Rais Karume inavyotoa mashirikiano yake kwa Umoja huo sanjari na Mashirika yake yaliopo hapa Zanzibar.

Dk. Migiro alimueleza Rais Karume kuwa licha ya kumaliza muda wake wa Urais yeye mwenyewe binafsi pamoja na UN hautamsahau Rais Karume kwa juhudi zake kubwa alizozifanya katika uongozi wake ikiwa ni pamoja na kuwaletea wananchi wa Zanzibar maendeleo makubwa.

Sambamba na hayo, Dk. Migiro aliipongeza Zanzibar kwa kuendelea kuunga mkono Umoja wa Mataifa.

Nae Rais Karume alitoa shukurani zake kwa UN na kueleza kuwa mashirikiano mazuri yamekuwa yakipatika kutoka Umoja huo kupitia mashirika yake yaliopo nchini yakiongozwa na UNDP.

Rais Karume alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inajivunia mashirikiano na uhusiano mwema unaoupata kutoka Umoja wa Mataifa ambapo alieleza kuwa hata katika mafanikio yaliopatikana kwenye zoezi la kura ya maoni Shirika la Maendeleo la UNDP lilitoa ushirikiano wake mkubwa katika ufanikishaji.

Katika maelezo yake, Rais Karume alisema kuwa Umoja wa Mataifa umekuwa karibu sana na Zanzibar katika kutoa mashirikiano yake kwenye kuimarisha miradi ya maendeleo na uchumi.

Akieleza juu ya mafanikio yaliopatikana katika kura ya maoni, Rais Karume alisema kuwa mafanikio ya kura ya maoni kwa Wazanzibari wote kwani lengo na madhumuni ni kuimarisha umoja,mshikamano sanjari na amani na utulivu.

Sambamba na hayo, Rais Karume alimueleza Naibu Katibu Mkuu huyo wa UN kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, inayokusudiwa kuundwa baada ya Uchaguzi Mkuu ujao ni ya wananchi wote wa Zanzibar.

Rais Karume alieleza kuwa Zanzibar imepata mafanikio kiuchumi, kisiasa na kijamii kutokana na mashirikiano mazuri yaliopo nchini, hivyo mafanikio hayo yataimarishwa zaidi kwa kukuza na kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa Wazanzibari.

Rais Karume alisema kuwa wananchi wa Zanzibar wamepiga hatua kidemokrasia hali ambayo imeonekana kutokana na maamuzi na mapendekezo yao waliyoyatoa katika kuimarisha umoja na mshikamano.

Katika mazungumzo hayo, Rais Karume alimueleza Naibu Katibu Mkuu huyo kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wananchi wake wanaipongeza UN chini na uongozi wa Bwana Ban Ki-moon kwa mashirikiano mazuri na uhusiano mwema unaotoa kwa Zanzibar.

EU YAIPONGEZA ZANZIBAR KWA KURA YA MAONI

UMOJA wa nchi za Ulaya (EU) umetoa pongezi kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Amani Abeid Karume kutokana na kufanikisha zoezi la Kura ya Maoni na kueleza kuwa Zanzibar imepata maendeleo ya kupigiwa mfano kidemokrasia.

Mwakilishi wa Umoja wa nchi za Ulaya, Balozi Tim Clarke aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na Rais Karume Ikulu mjini Zanzibar.

Katika mazungumzo hayo ambapo Balozi Clarke akifuatana na baadhi ya Mabalozi wa nchi za Ulaya wanaofanyia kazi zao hapa Tanzania, alisema kuwa hatua iliyofikiwa Zanzib ar katika demokrasia ni kubwa na inapaswa kuungwa mkono.

Alisema kuwa Umoja wa nchi za Ulaya umeridhishwa na hatua hiyo na kutoa pongezi zake kwa Rais Karume pamoja na Wazanzibari wote kwa jumla kutokana na mafanikio makubwa waliyoyapata katika kuimarisha demokrasia.

Bwana Clarke na ujumbe wake walimueleza Rais Karume kuwa wanamatarajio makubwa kuwa Zanzibar itazidi kupiga hatua katika kuimarisha maendeleo yake sanjari na kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi wake hali ambayo itaipaisha Zanzibar katika medani na kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mwakilishi huyo, alimueleza Rais Karume kuwa ulimwengu mzima kwa namna zoezi hilo lilivyoendeshwa na hatimae kumalizika kwa ufanisi.

Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walimueleza Rais Karume kuwa wameridhika na kuvutika kwa namna ya zoezi zima la Kura ya Maoni lilivyokwenda vizuri na kuwa ulimwengu mzima umefurahishwa na namna lilivyokwenda kwa amani na utulivu.

Walieleza kuwa EU itaendelea kutoa mashirikiano yake na Zanzibar kwa na kueleza kuwa wanamatumaini makubwa kuwa Umoja na mshikamano wa Wazanzibari utaendelea kuimarika zaidi.

Aidha, viongozi hao, walimueleza Rais Karume kuwa ni kiongozi anaependa umoja, mshikamano sanjari na kuimarishaji amani na utulivu hapa nchini kwa lengo la kuiletea Zanzibar maendeleo na maisha yenye utulivu.

Sambamba na hayo, viongozi hao waliwatakia Wazanzibari wote pamoja na viongozi wao wa kisiasa kuendelea kupata mafanikio katika kutekeleza umoja huo kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi na nchi yao kwa jumla.

Viongozi hao waliahidi kushirikiana bega kwa bega na Zanzibar katika kuhakikisha mafanikio zaidi yanapatikana katika kuimarisha sekta za maendeleo kutokana na kuthamini juhudi inazozichukua katika kufikia hatua hiyo..

Nae, Rais Karume kwa upande wake aliwaeleza viongozi hao wa EU kuwa zoezi la kura ya maoni ni la kihistoria ambalo limewapa wananchi wa Zanzibar haki ya kushiriki kikamilifu katika maamuzi wanayohisi yatawaletea manufaa zaidi.

Alieleza kuwa katika zoezi hilo la Kura ya Maoni hakuna alieshinda na aliyeshindwa kwani washindi ni Wazanzibari wote ambao wanapenda amani, umoja na mshikamano.

Rais Karume alieleza kuwa mafanikio ya zoezi hilo yamedhihirisha wazia kuwa Wazanzibari wamepevuka kisiasa.

Rais Karume alisema kuwa Wazanzibari wote wanapenda umoja, mshikamano sanjari na amani na utulivu na ndio maana wameunga mkono ili kutimiza na kuendeleza malengo yao hayo.

“Watu wote wa Zanzibar wanapenda amani”,alisema Rais Karume. Aidha, Rais Karume alisema kuwa kwenda vizuri kwa zoezi hilo kunatokana na taratibu nzuri zilizowekwa na Tume husika sanjari na wananchi wenyewe kuwa na mwamko na uwelewa juu ya zoezi hilo.

Katika mazungumzo hayo, Rais Karume alisema kuwa kufanikiwa kwa zoezi hilo kutatoa matokeo mazuri ambayo yataijenga Zanzibar mpya na yenye amani, umoja na mshikamano.

Rais Karume alitoa pongezi na shukurani kwa Washirika wa Maendeleo zikiwemo nchi za Umoja wa Ulaya kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo sanjari na kuunga mkono zoezi la Kura ya Maoni lililofanyika Julai 31 mwaka huu.

MAWAZIRI WATANO WA SMZ WATUPWA CHINI KWENYE KURA YA MAONI

Viongozi wandamizi wakuu watano wa serikali ya mapinduzi Zanzibari ni miongoni mwa wagombea waliokataliwa kugombea nafasi za uwakilishi katika uchaguzi mkuu kupita chama cha mapinduzi CCM.
Kwa mujibu wa matokeo ya kura hiyo iliyopigwa siku ya Jumapili waliokataliwa nafasi ya uwakilishi ni waziri wa Kilimo, Mifugo na Mazingira, Burhan Saadat Haji jimbo la Kikwajuni na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Sultani Mohammed Mugheiry jimbo la Mji Mkongwe.
Wengine ni naibu waziri wa kilimo Khatib Suleiman jimbo la Bububu, naibu waziri wa maji, ujenzi nishati na ardhi Tafana Kassim Mzee jimbo la Uzini na naibu waziri wa mawasiliano na uchukuzi, Mzee Ali Ussi jimbo la Chaani.
Nae mwenyekiti wa zamani wa umoja wa vijana wa CCM taifa Hamad Masauni aliekumbwa na kashfa ya kuhushi umri wake ameshinda kuwania nafasi ya ubunge jimbo la Kikwajuni, huku naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar Saleh Ramadhan Ferouz akiambulia nafasi ya tatu.
Hata hivyo mawaziri wengine akiwemo waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha jimbo la Mwanakwerekwe na waziri wa elimu na mafunzo ya amali Haroun Suleiman Ali jimbo la Makunduchi wamechaguliwa tena kugombea nafasi ya uwakilishi.
Mawaziri wengine walioshinda katika kura hiyo ni Naibu waziri Kiongozi Ali Juma Shamuhuna jimbo la Donge, waziri wa Maji Ujenzi Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid jimbo la Kiembesamaki na Waziri anaeshugulikia fedha na Uchumi Dk. Mwinyihaji Makame jimbo la Dimani.
Waziri wa Utalii Biashara na Uwekezaji, Samia Suluhu Hassan ameshinda nafasi ya Ubunge jimbo la Makunduchi, waziri wa mawasiliano na uchukuzi Machano Othman Said ameshinda nafasi ya uwakilishi jimbo la Chumbuni.
Aidha waziri wa nchi ofisi ya waziri kiongozi, Hamza Hassan Juma ameshinda nafasi ya uwakilishi jimbo la Kwamtipura.
Mawaziri wa Serikali ya Muungano wanaoendelea kutetea nafasi zao ni Dr. Hussen Mwinyi jimbo la Kwahani, naibu waziri wa mambo ya nje na ushirikiano Balozi Seif Ali Idd jimbo la Kitope na waziri anaeshughulikia masuala ya muungano Mohammed Seif Khatib jimbo la Uzini.
Katibu wa CCM wilaya ya Mjini Magharibi, Fatma Shomari amesema wagombea wengi walioshindwa katika kinyanganyiro hicho cha kura za maoni wamewasilisha malalamiko kwa kutoridhika jinsi ya

ZANZIBAR KUUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

Wananchi wa Zanzibar wamekubali muundo mpya wa serikali ya umoja wa kitaifa baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu kufuatia kupiga kura ya maoni ya ndio kwa asilimia 66.4 iliyofanyika jana.
Akitangaza matokeo hayo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Khatib Mwinyichande amesema wananchi waliopiga kura ya ndio ni laki moja, 88 elf, 705 sawa na asilimia 66.4.
Kura za hapana ni elfu 95, 613 sawa na asilimia 33.6, kura zilizoharibika ni elfu nane 721 sawa na asilimia 3.0 kati ya wananchi waliopiga kura laki mbili, elfu 93 na 36 sawa na asilimia 71.9.
Kwa mujibu wa matokeo hayo Mwinyichande amewatangaza wananchi waliopiga kura ya ndio wameshinda katika kura ya maoni kwa asilimia 66.4…

Akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kutolewa matokeo hayo hoteli ya Bwawani katibu mkuu wa CUF Seif Sharif Hamad amesema kura hiyo inaonesha wazanzibar wametaka kusahau yaliopita.
Amesema ushindi huo ni wa wazanzibari wote na kwamba matumaini yake ni kuanza ukurasa mpya kwa kuijenga Zanzibar mpya na kuwataka wananchi kushirikiana ili kuiletea maendeleo nchi yao….
Nae naibu katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Saleh Ramadhan Ferouz amesema matokeo hayo yametoa picha juu ya wazanzibari wanaotaka kuungana katika kuijenga Zanzibar.
Aidha amewataka wananchi kuufanya uchaguzi mkuu

Sunday, July 11, 2010

SHENI AKATA TIKETI YA KUGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR KWA TIKETI YA CCM


Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Ali Mohamed Shein akiwashukuru wajumbe wa Halmashauri kuu ya taifa CCM kwa kumchagua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM.


Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa na wajumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa CCM kuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika ukumbi wa White house mjini Dodoma jana usiku.

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Dr.Gharib Bilal kwa kukubali matokeo ya ushindi wa Dr.Ali Mohamed Shein kuwania urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM jana usiku.

Wednesday, June 23, 2010

MKATABA WA MUUNGANO WADAIWA BUNGENI

Kambi ya upinzani bungeni imeomba kupatiwa mkataba wa asili wa muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ambao unaweza kuyapatia ufumbuzi baadhi ya matatizo yaliomo kwenye muungano huo.

Akizungumza na Zenji Fm radio msemaji wa kambi hiyo katika mambo ya muungano Riziki Omar Juma amesema serikali bado inashikilia mkataba huo na hauwekwi wazi kwa wananchi.

Amesema mkataba huo tayari umeshadaiwa ndani ya bunge na serikali kuahidi kwamba mbunge yoyote anaweza kuuona, lakini hadi sasa bado mkataba huo umekuwa siri.

Riziki amesema lengo la kutaka kuonekana mkataba huo ni kutaka kuufanyia marekebisho kama utaonekana kuwa na kasoro ili kila upande unufaike na maslahi ya muungano…..

Akizungumza na Zenji Fm radio juu ya madai hayo waziri wa muungano Mohammed Seif Khatib amesema mikataba hiyo iko ikulu ya rais mjini Zanzibar na ikulu ya rais wa muungano mjini Dar es Salaam.

Hata hivyo amesema hati hizo zinakuwa na umuhimu pale sheria na katiba hazijaundwa na baada ya vitu hivyo kuwepo mikataba hiyo haina umuhimu sana kama inavyodaiwa…

Hivi karibuni kumejitokeza baadhi ya kikundi cha watu wanaodai hati halisi ya muungano na kutishia kufungua kesi katika mahakama ya umoja wa mataifa baada madai yao kutupiwa mbali na mahakama kuu ya Zanzibar.

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA MABALOZI

Rais Jakaya Kikwete amefanya uteuzi na kuwahamishia vituo vyao vya kazi mabalazi saba kushika nyadhifa mbali mbali za kibalozi nje ya Tanzania.

Mabalozi hao ni pamoja Mohammed Mwinyi Mzale anaekuwa balozi wa Tanzania nchini Sweeden, Alexanda Masinda anaekwenda nchini Canada, Peter Alen Nkalage anakuwa balozi mpya nchini Uingereza.

Dansan Joram anaekuwa balozi wa Tanzania nchini Etheopia, Egum Karim Haji anaekwenda Ufaransa na balozi Ombeni Chubuwe ameteuliwa kuwa mwakilishi wa kudumu katika umoja wa mataifa.

Dr. Omar Mohammed aliekuwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na umoja wa Afrika amerejeshwa nchini atakuwa mkuu wa chuo cha Diplomasia mjini Dar es Salaam.

MKUZA WALETA MAFANIKIO Z’BAR

Mpango wa kukuza uchumi na kuimarisha umasikini Zanzibar umelezewa kupata mafanikio katika sekta ya kilimo na biashara.

Akizunguma na Zenji Fm radio mchumi wa Zanzibar Dr. Mohammed Hafidhi amesema inagawa wananchi wanahitaji maendeleo makubwa zaidi kuliko hayo yaliofikiwa.

Amesema mafanikio hayo yanatokana na kuliweza baraza la biashara la Zanzibar kufanaya kazi zake vizuri kumeziwezesha sekta za kilimo na biashara kupiga hatua kubwa za maendeleo.

Aidha amesema MKUZA pia umesaidia kuendeleza sekta ya ufugaji kwa kuanzisha miradi mbali mbali kama vile PADEP, ASP pamoja na kutoa mafunzo ambayo lengo lake ni kuendeleaza wafugaji.

Hata hivyo Dr. Hafidh amesema bado mpango huo uanakabiliwa na changamoto ikiwemo kudhorota kwa sekta ya viwanda, uvuvi na kuongeza wigo wa mapato ya serikali

WAGOMBEA URAIS CCM WACHUKUA FOMU LEO

anachama Saba wa chama cha Mapinduzi CCM, tayari wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho katika afisi kuu ya CCM Kisiwandui.

Wanachama hao ni waziri kiongozi Shamsi Vuai Nahodha, makamo wa rais Dr. Ali Mohammed Shein, waziri kiongozi wa zamani Dr. Mohammed Gharib Bilal na naibu waziri kiongozi Ali Juma Shamhuna.

Wengine ni naibu waziri wa Afrika mashariki Mohammed Aboud, balozi Ali Abeid Karume na kamishna mstaafu wa utamaduni Hamad Bakar Mshindo.

Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti wagombea hao wametaja kuimarisha sekta za maendeleo zikiwemo elimu, kilimo, miundo mbinu ya usafiri pamoja na kuondoa malumbano ili kuwaunganisha wazanzibari kuwa kitu kimoja.

Wamesema Zanzibar bado inakabiliwa na changamoto za kiuchumi hivyo watajenga mazingira mazuri ikiwani pamoja na kuimarisha sekta za kazi ili kutoa huduma nzuri pamoja na kubuni nafasi za ajira.

Aidha viongozi hao wamesema wataendelea kuimarisha muungano ili kuleta mafanikio zaidi kwa wananchi na kuendelea kuyapatia fumbuzi baadhi ya matatizo yaliosalia kwa lengo la kuleta maslahi kwa pande zote mbili.

Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi fomu wagombea hao katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Vuai Ali Vuai amesema kamati kuu ya halamshauri itapitia sifa za wagombea hao na kutoa mapendekezo yake kwa majina matatu kwa halmashauri kuu ya taifa kwa uteuzi wa mwisho…

Afisi kuu ya CCM bado inaendelea kutoa fomu kwa wanachama wengine wanaotaka kuwania urais wa Zanzibar kupitia chama hicho hadi Julai mosi mwaka huu.

Idadi hiyo ya wananchama waliojitokeza kuchukua fomu ya kukiomba chama chao kuwateuwa kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar ni kubwa ikilinganishwa na wanachama waliojitokeza kumrithi rais wa zamani Dr. Salmin Amour Juma mwaka 2000.

Wachambuzi wa masuala ya siasa Zanzibar wanasema uchaguzi wa rais mwaka 2010 utakuwa na upinzani mkali na vyama vikuu viliwi vya siasa vyenye wafuasi wengi CCM na CUF vitahitaji kufanya kazi ya ziada.

SERIKALI YA MSETO Z’BAR YAUNGWA MKONO NA WAISLAM

Jumuiya ya Maimamu Zanzibar JUMAZA imesema inaunga mkono kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa kama hatua moja wapo ya kuimarisha amani na utulivu nchini.

Katibu Mtendaji wa JUMAZA sheikh Muhdin Zuber Muhdini amesema hatua hiyo ni kuzishukuru neema za mwenyezi mungu zilizoondosha siasa za chuki zilizoleta mirafarakano na uadui

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa amesema serikali ya umoja wa kitaifa ndio suluhisho la kuleta amani, hivyo amewataka wananchi kushiriki katika kura ya maoni ili kutoa ridhaa ya kuundwa serikali hiyo…

Hata hivyo Sheikh Muhidin amesema jumuiya hiyo haiwezi kuwalazimisha wananchi kutumia uhuru wao wa kuamua, lakini jumuiya za waislamu zinajukumu la kuielekeza jamii umuhimu wa kulinda amani na utulivu.

Aidha jumuiya hiyo pia imewataka wananchi kuendeleza amani na utulivu uliopo hasa wakati huu wa kuelekea uchaguzi wa kuwachagua viongozi mbali mbali wa nchi.

Tamko hilo la JUMAZA la kuunga mkono kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa limefikiwa katika kikao chake kilichofanyika June 12 mwaka huu na kuzishirikisha jumla ya taasisi 18 za kislamu

Saturday, June 19, 2010

MABADILIKO YA HALI YA HEWA HAYATAIATHIRI Z,BAR

izara ya kilimo mifugo na mazingira imesema tishio la dunia la kuzama kwa visiwa vidogo duniani miaka 50 ijayo kutokana na uharibifu wa mazingira halivihusu visiwa vya Zanzibar.

Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi naibu waziri wa wizara hiyo Khatib Suleiman Bakar amesema tishio hilo limetolewa kwa visiwa vya Maldives na sio visiwa vya Zanzibar.

Hata hivyo amesema wizara imekuwa ikitoa elimu ya kuhifadhi mazingira juu ya athari za mabadiliko ya hali ya hewa kutokana nakupanda kwa kina cha bahari katika baadhi ya vijiji vya ukanda wa pwani

Akijibu suala la nyongeza waziri wa wizara hiyo Burhan Saadat Haji amesema serikali inamalizia utafiti wa kupitia visiwa vyote vya Unguja na Pemba ili kuangalia maeneo yalioathirika na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

Amesema mara baada ya kumalizika utafiti huo serikali itaangaliza uwezekano wa kudhibiti maeneo yanayovamiwa na maji ya bahari hasa maeno ya kilimo Pemba kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo…

WALIOKOSA KUJIANDIKISHA WASTAHAMILI-HAMZA

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewataka watu waliokosa kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura wastahamili hadi pale tume ya uchaguzi itakapofanya usajili kwa ajili ya chaguzi nyingine. Waziri wa nchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma amesema, hivi sasa tume ya uchaguzi haina muda tena wa kurudia kazi za uandikishaji baada ya kumalizika wamu tatu tofauti za usajili.

Akijibu maswali katika kikao cha baraza la wawakilishi Juma amesema tume imefanikiwa kuandikisha zaidi ya asilimia 80 idadi ambayo ni kubwa ikilinganishwa na nchi zilizoendelea

Aidha waziri Juma amesema idadi ya wapiga kura katika uchaguzi wa mwaka 2010 ni ndogo ikilinganishwa na mwaka 2005 inatokana na hiari mtu mwenyewe kujiandikisha au la kutumia teknolojia inayozuwia watu kujiandikisha zaidi ya mara moja.

Hata hivyo amesema watu waliobainika kujiandikishwa mara mbili, watapata haki ya kupiga kura, lakini watafikishwa mahakamani kutokana na kukiuka taratibu za uandikishaji……

Tume ya uchaguzi Zanzibar imeandikisha wapiga kura laki nne, 8,401 katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba mwaka huu wakati idadi ya watu waliopata vitambulisho vya ukaazi ni zaidi ya laki tano

CCM ZANZIBAR WAJITOKEZA KUWANIA URAIS 2010

Wanachama sita wa chama cha Mapinduzi CCM wamejitokeza kutaka kuwania kiti cha urais wa Zanzibar kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba mwaka huu.

Wanachama hao waliojitokeza ni makamo wa rais Dr. Ali Mohammed Shein, waziri kiongozi wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha na waziri kiongozi wa zamani Dr. Mohammed Gharib Bilal.

Wengine ni naibu waziri kiongozi Ali Juma Shamhuna, balozi Ali Abeid Karume na Hamad Bakar Mshindo.

Akiwasilisha majina hayo kwa wandishi wa habari katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Vuai Ali Vuai amesema wanachama hao watachukua fomu siku ya Jumatatu na kusema shughuli hiyo haitakuwa na sherehe.

Amesema fomu za kuwania nafasi hiyo zitaendelea kutolewa kuanzia tarehe 21 mwezi huu hadi Julai mosi kwa wananchama wengine wanaotaka kuwania nafasi hiyo kupitia CCM na kurejesha ndani ya kipindi hicho.

Vuai amesema wanachama hao watalipia fomu hiyo shilingi milioni moja na mwisho wa kurejesha fomu hiyo Juali mosi saa 10.00 jioni ikiwa na wadhamini 250 kutoka mikoa yote ya Zanzibar.

Amesema afisi bado inaendelea kuwakaribisha wanachama wengine watakaokuwa tayari kuchukua fomu za kuwania urais wa Zanzibar kupitia CCM.

Miongoni mwa wanachama wa CCM wanaotajwa kuwania nafasi hiyo akiwemo

Ali Juma Shamhuna

naibu waziri wa Afrika mashariki Mohamed Aboud, waziri wa muungano Mohammed Seif Khatib na waziri wa Elimu Haroun Ali Suleiman bado hawajajitokeza hadharani kutangaza nia zao za kuwania nafasi hiyo.

Waziri kiongozi wa zamani Dr. Gharib hii ni mara yake ya tatu kukiomba chama chake kumteuwe kuwania urais wa Zanzibar ambapo mwaka 2005 aliombwa kujiondoa ili kumwachia rais Karume aendelee na kipindi cha pili cha miaka mitano kinachotarajiwa kumalizika Octoba mwaka huu

MAHAKAMA YA RUFAA TANZANIA IMESEMA MGOMBEA BINAFSI NI SUALA LA KISIASA

Mahakama ya Rufaa nchini imesema haina mamlaka ya kuamua juu ya mgombea binapsi na kwamba mwenye mamlaka wa kuamua hilo ni Bunge na wananchi wenyewe .

Uamuzi huo umetolewa chini ya jopo la majaji saba likiongozwa na Jaji mkuu Agostino Ramadhan katika mahakama ya Rufaa jijini Dar es salaam.

Mahakama hiyo imesema suala hilo ni la kisiasa zaidi na si lakisheria hivyo uamuzi zaidi unahitajika kutolewa na wananchi wenyewe na kueleza kuwa uamuzi huo utakao tolewa ni vyema kuzingatia historia ya Tanzania na matakwa ya wananchi.

MSAMAHA WA KIKWETE HAUHUSU WAFUNGWA WA ZANZIBAR-SMZ

erikali ya mapinduzi Zanzibar imesema msamaha wa wafungwa unaotolewa na rais wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania hauhusu wafungwa walioko katika vyuo vya mafunzo vya Zanzibar.

Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi waziri wa nchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma amesema kila upande wa muunganoi una mamlaka yake , hivyo rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ndio mwenye mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa walioko Zanzibar na rais wa mungano anatoa msamaha kwa wafungwa walioko Tanzania bara.

Amesema licha ya Tanzania kuwa na mahakama moja ya rufaa inayoziunganisha nchi zote mbili, lakini wananchi watakaopatikana na hatia na kupewa adhabu ya kifungo wafungwa watapewa misahama kwa majibu wa mamla wa nchi hizo mbili.

Nae waziri kiongozi Shamsi Vuai Nahodha akiongezea majibu ya suala hilo amesema katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na katiba ya Zanzibar kuna mgawanyo maalumu ya mamlaka kulinga na makubaliano ya pande mbili za muungano.

Hivyo hivyo amesema serikali haitapanua wigo ambao unaweza Zanzibar kunyimwa mamlaka yake

Wednesday, June 16, 2010

LIBENEKE LA MTANZANIA AKIWA INDIA


www.allyshams.blogspot.com

TASAF KULETA MATUMAINI TANZANIA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Amani Abeid Karume amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zote kwa pamoja zimepanga mikakati maalum kwa ajili ya kuwapunguzia wananchi wake makali ya umasikini.

Rais Karume aliyasema hayo leo katika ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa kuhusu miradi ya jamii kwa nchi zinazoendelea unaofanyika katika ukumbi wa Mkutano wa AICC Mjini Arusha.

Rais Karume ambaye alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, alieleza kuwa Serikali zote mbili za Tanzania zinatambua umuhimu wa kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), ambao huwashirikisha wadau wengi.

Alieleza kuwa katika kipindi chote ambacho TASAF imekuwa ikifanya kazi jumla ya miradi 11,375 ya jamii imepatiwa misaada kutoka mfuko huo wenye thamani ya Dola za Kimarekani 164,446,823.

Rais Karume alieleza kuwa kati ya miradi yote iliyopata misaada kutoka TASAF 928 ilikuwa ni kwa ajili ya kazi za kijamii yenye thamani ya Dola za Kimarekani 21,422,495.28 iliyowanufaisha jumla ya watu 217,315.

“Tokea kuanzishwa kwa TASAF tayari umeshawanufaisha watu 15,320,58 ambao wameweza kuzitumia huduma zilizotolewa baada ya kukamilika kwa miradi ya kijamii katika maeneo yao”,alieleza Rais Karume.

Aidha, Rais Karume alisema kuwa TASAF imekuwa ikifanya kazi vizuri Zanzibar na tayari imeshatoa kiasi cha Dola za Kimarekani 2.50 milioni kwa ajili ya kusaidia miradi mbali mbali maendeleo katika awamu ya pili iliyoanza mwaka 2005.

Pia, Rais Karume iliisifu TASAF kwa misaada midogo midogo inayotolewa kutoka katika Mfuko huo.

“Mahitaji ya familia yanaongezeka lakini kipato hakiongezeki, kutokana na sababu hii Serikali ya Tanzania imetambua umuhimu wa kuanzisha mfuko wa Mandeleo ya Jamii (TASAF), ambapo matatizo mbali mbali yanayozikabili jamii yamekuwa yakishughulikiwa kwa kiasi kikubwa”,alisisitiza Rais Karume.

Alieleza kuwa Mpango wa Maendeleo wa muda mrefu wa Dira ya 2025 kwa Tanzania Bara na ule wa 2020 kwa Zanzibar unatambua umuhimu wa kuwawezesha watu mbali mbali katika makundi tofauti wakiwemo wale wanaoishi katika mazingira magumu.

Akihutubia katika mkutano huo unaohudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 45 duniani, Rais Karume alisema kuwa mkutano huo unafanyika wakati dunia ikiwa katika jitihada kubwa ya kutatua matatizo yaliyojitokeza kutokana na kutetereka kwa uchumi na mfumo wa fedha wa duniaambao umeathiri shughuli za kibiasahara na kushuka kwa sekta ya uwekezaji duniani.

Rais Karume alieleza kuwa pale uchumi wa dunia unaposhuka matatizo yanayotokea katika mataifa makubwa yenye nguvu za kiuchumi athari zinazotokezea huzikumba na nchi ndogo..

Alieleza kuwa miongoni mwa athari hizo ni pamoja na kuwepo kiwango kidogo cha uwekezaji na kutetereka kwa sekta ya Utalii ambapo nako kumechangia kushuka kwa soko la ajira na mapato ya serikali ambapo pia, imepelekea kuathiri utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya kijamii.

Nae Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Utawala Bora Mhe. Sophia Simba alieleza kuwa TASAF imekuwa na umuhimu mkubwa katika kuimarisha shughuli za maendeleo ya kijamii hapa Tanzania na kuishukuru Benki ya Dunia kwa uwamuzi wake wa kufanya mkutano wake huo muhimu hapa nchini.

Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bwana John Murray McIntire alieleza kuwa Benki ya Dunia itaendelea kuunga mkono katika kufanikisha Miradi ya TASAF kwa kutambua umhimu wake katika maendeleo ya jamii.

Alieleza kuwa miongoni mwa nchi zilizopata mafanikio katika Mfuko huo wa TASAF ni pamoja na Tanzania ambayo imeweza kuimarisha miradi mbali mbali ya maendeleo.

Wakati huo huo Rais Karume alikagua maonyesho yaliyotayarishwa na TASAF na kuona jinsi mfuko huo unavyofanya kazi kutokana na maelezo aliyokuwa akipewa na watayarishaji husika