I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, October 31, 2010

ZANZIBAR YAFANYA UCHAGUZI KWA AMANI NA UTULIVU

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania umeanza vizuri, licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo zilizosababisha baadhi ya majimbo ya matatu ya ubunge na wadi tisa kwa Zanzibar kutofanyika kutokana na hitilafu za karatasi za kupigia kura. Miongoni mwa wadi zilizoahirishwa uchaguzi huo ni Kajengwa, Mangapwani, Mchangani, Kwahani Miembeni, Nyerere na wadi tatu za Pemba na majimbo yaliohirishwa uchaguzi ni Mtoni, Mwanakwerekwe na Magogoni. Mwandishi wetu alietembelea vituo vya kupigia kura Mwanakwerekwe amesema baadhi ya mawakala wamelalamikia uhaba wa vitabu vya kupigia vya urais wa jamhuri ya muungano. Wakala wa CUF katika kituo cha Mwanakwerekwe amesema vitabu vilivyotarajiwa kuwepo katika vituo hivyo ni vitano, lakini vimefika vitatu hivyo kuna uwezekano kwa watu wengine kukosa kupiga kura. Akizungumzia suala hilo mkurugenzi wa tume ya uchaguzi Tanzania Rajab Kiravu amesema tayari makamishna wa tume hiyo wanafuatilia matatizo hayo katika vituo vya Tanzania bara na Zanzibar…

Nae mgombe mwenza wa chama cha ATPP-MAENDELEO Rashid Mchenga amesema iwapo baadhi ya wananchi watakosa kupiga kura kutokana na uchache wa vitabu uchaguzi utarejewe kulingana na sheria Hata hivyo akizungumza na Zenji Fm radio amesema uchaguzi umefanyika kwa amani na utulivu na kuwataka wagombea kukubali matokeo kwa maslahi ya taifa lao…

Na huko Tanzania bara baadhi ya wapiga kura mjini Dar es Salaam walilalamika tatizo la kutokuwemo kwa majina yao katika orodha ya wapiga kura. Kazi za kuhesabu kura zinatarajiwa kuanza katika vituo vyote vya kupigia kura na matokeo yake yatabandikwa katika vituo hivyo

No comments:

Post a Comment