I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, October 31, 2010

MAALIM SEIF AHIDI KUKUBALI MATOKEO YA UCHAGUZI

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF Seif Sharif Hamad amesema yuko tayari kukubali matokeo ya uchaguzi na kuwataka wafuasi wa chama hicho kutiofanya vurugu wakati wa kutangazwa matokeo hayo.

Hata hivyo mgombea huyo ametoa wito kwa tume ya uchaguzi Zanzibar kuendesha uchaguzi wa haki na huru na kuwasimamia maafisa wake wa wilaya ambao wanatiliwa shaka ya kutaka kuchafua uchaguzi.

Akizungumza katika mkutano wa mwisho wa kampeni za uchaguzi huko viwanja vya Maisara Maalim Seif amesema wakati umefika kwa wazanzibar kuachana na siasa za chuki na kuanza kutafuta njia za kujiiinua kimaendeleo.

Amesema wazanzibar wana kila sababu ya kuendeleza maridhiano ya kisiasa yanayolenga kuijenga Zanzibar mpya

Kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa itakayoundwa baada ya uchaguzi amesema endapo ataingia madarakani atahakikisha serikali hiyo inawajumuisha wazanzibari wote bila kujali udini na ukabila.

Amesema ataingoza Zanzibar kwa kutumia utawala wa sheria na hakuna kiongozi hata mmoja atakaekuwa juu ya sheria ili kuona kila mwananchi anapata haki yake.

Aidha mgombea huyo amesema endapo wananchi watamchagua serikali yake itaimarisha uchumu kwa asilimia 15 utakaolenga kuinua maisha ya wananchi kwa kuongeza nafasi za ajira.

No comments:

Post a Comment