I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 23, 2010

MKUZA WALETA MAFANIKIO Z’BAR

Mpango wa kukuza uchumi na kuimarisha umasikini Zanzibar umelezewa kupata mafanikio katika sekta ya kilimo na biashara.

Akizunguma na Zenji Fm radio mchumi wa Zanzibar Dr. Mohammed Hafidhi amesema inagawa wananchi wanahitaji maendeleo makubwa zaidi kuliko hayo yaliofikiwa.

Amesema mafanikio hayo yanatokana na kuliweza baraza la biashara la Zanzibar kufanaya kazi zake vizuri kumeziwezesha sekta za kilimo na biashara kupiga hatua kubwa za maendeleo.

Aidha amesema MKUZA pia umesaidia kuendeleza sekta ya ufugaji kwa kuanzisha miradi mbali mbali kama vile PADEP, ASP pamoja na kutoa mafunzo ambayo lengo lake ni kuendeleaza wafugaji.

Hata hivyo Dr. Hafidh amesema bado mpango huo uanakabiliwa na changamoto ikiwemo kudhorota kwa sekta ya viwanda, uvuvi na kuongeza wigo wa mapato ya serikali

No comments:

Post a Comment