I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 16, 2010

TAKUKURU KUWA CHUKULIA HATUA WAGOMBEA WANAOTOA ZAWADI

Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kupambana na rushwa TAKUKURU Dr. Eduward Husea amesema taasisi hiyo inazifanyia kazi taarifa za wagombea wa nafasi mbali mbali katika uchaguzi mkuu ujao walioanza kutoa vitu kama zawadi.

Akizungumza na wahariri wa habari katika semina juu ya sheria mpya ya uchaguzi mjini Dar es Salaam amesema taarifa za wagombea hao zitakapokamilika wataanza kuchukuliwa hatua za kisheria.

Aidha amesema suala hilo litachukua muda mrefu kutokana na kuthibitisha tuhuma hizo na kusema sheria hiyo itasaidia kuzuwia na kupambana na rushwa wakati wa uchaguzi ili kuwapata viongozi safi na waadilifu.

Aidha dr. Husea amesema ni kinyume cha sheria kwa baadhi ya watu kutumia madhehebu ya dini kama maeneo ya kufanyia kampeni na watakapobainika sheria itachukua mkondo wake.

No comments:

Post a Comment