I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, June 1, 2010

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU TUNGUU ZAIDI 300 WAMEFUKUZWA KWA KUSHINDWA KULIPA ADA

KOA WA KUSINI UNGUJA: Wanafunzi wa chuo kikuu cha Zanzibar, Tunguu mwaka wa pili, wameulalamikia uongozi wa chuo hicho kuwafukuza baada ya kukosa kusajiliwa kwa kile kilichoelezwa kushindwa kukamilisha malipo ya ada. Akizungumza na Zenji Fm radio mmoja wa wanafunzi hao amedai chuo hicho kimeongeza ada ya masomo kinyume na mkataba wao wa zamani hivyo wameshindwa kulipa ada hiyo na kulazimika kufukuzwa. Amedai kutokana na kufukuzwa chuo kinyume na sheria wanatarajia kufungua kesi mahakamani wiki ijayo kutokana na kufukuzwa kwa zaidi ya wanafunzi Hata hivyo uongozi wa chuo hicho haukuweza kupatikana kuelezea juu ya madai hayo ya wanafunzi kufukuzwa chuoni hapo

No comments:

Post a Comment