I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 23, 2010

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA MABALOZI

Rais Jakaya Kikwete amefanya uteuzi na kuwahamishia vituo vyao vya kazi mabalazi saba kushika nyadhifa mbali mbali za kibalozi nje ya Tanzania.

Mabalozi hao ni pamoja Mohammed Mwinyi Mzale anaekuwa balozi wa Tanzania nchini Sweeden, Alexanda Masinda anaekwenda nchini Canada, Peter Alen Nkalage anakuwa balozi mpya nchini Uingereza.

Dansan Joram anaekuwa balozi wa Tanzania nchini Etheopia, Egum Karim Haji anaekwenda Ufaransa na balozi Ombeni Chubuwe ameteuliwa kuwa mwakilishi wa kudumu katika umoja wa mataifa.

Dr. Omar Mohammed aliekuwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na umoja wa Afrika amerejeshwa nchini atakuwa mkuu wa chuo cha Diplomasia mjini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment