I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, June 19, 2010

MAHAKAMA YA RUFAA TANZANIA IMESEMA MGOMBEA BINAFSI NI SUALA LA KISIASA

Mahakama ya Rufaa nchini imesema haina mamlaka ya kuamua juu ya mgombea binapsi na kwamba mwenye mamlaka wa kuamua hilo ni Bunge na wananchi wenyewe .

Uamuzi huo umetolewa chini ya jopo la majaji saba likiongozwa na Jaji mkuu Agostino Ramadhan katika mahakama ya Rufaa jijini Dar es salaam.

Mahakama hiyo imesema suala hilo ni la kisiasa zaidi na si lakisheria hivyo uamuzi zaidi unahitajika kutolewa na wananchi wenyewe na kueleza kuwa uamuzi huo utakao tolewa ni vyema kuzingatia historia ya Tanzania na matakwa ya wananchi.

No comments:

Post a Comment