I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, June 7, 2010

IRAN IMEAHIDI KUISAIDIA ZANZIBAR

Serikali ya Iran imeahidi kuisaidia Zanzibar katika kuimarisha sekta za elimu, kilimo na uvuvi.

Naibu waziri wa mambo ya nje wa Iran Dr. Harith Suleiman amesema Zanzibar inayonafasi nzuri ya kuvutia wawekezaji katika sekta hizo, hivyo serikali yake itaongeza nafasi za masomo nchini Iran kwa vijana wa Zanzibar.

Akizungumza na waziri kiongozi Shamsi Vuai Nahodha amesema Iran pia itaisaidia Zanzibar kuimarisha kilimo cha umwagiliaji maji na uvuvi wa bahari kuu na hospitali ya kitalii na watu mashughuri.

Nae waziri kiongozi Nahodha amesema upatikanaji wa uemem nchini utasaidia juhudi za serikali za kukabiliana na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na wananchi.

No comments:

Post a Comment