I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, June 19, 2010

MABADILIKO YA HALI YA HEWA HAYATAIATHIRI Z,BAR

izara ya kilimo mifugo na mazingira imesema tishio la dunia la kuzama kwa visiwa vidogo duniani miaka 50 ijayo kutokana na uharibifu wa mazingira halivihusu visiwa vya Zanzibar.

Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi naibu waziri wa wizara hiyo Khatib Suleiman Bakar amesema tishio hilo limetolewa kwa visiwa vya Maldives na sio visiwa vya Zanzibar.

Hata hivyo amesema wizara imekuwa ikitoa elimu ya kuhifadhi mazingira juu ya athari za mabadiliko ya hali ya hewa kutokana nakupanda kwa kina cha bahari katika baadhi ya vijiji vya ukanda wa pwani

Akijibu suala la nyongeza waziri wa wizara hiyo Burhan Saadat Haji amesema serikali inamalizia utafiti wa kupitia visiwa vyote vya Unguja na Pemba ili kuangalia maeneo yalioathirika na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

Amesema mara baada ya kumalizika utafiti huo serikali itaangaliza uwezekano wa kudhibiti maeneo yanayovamiwa na maji ya bahari hasa maeno ya kilimo Pemba kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo…

No comments:

Post a Comment