I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, June 5, 2010

MSANII MAARUFU WA TANZANIA YUSSUF AHMMED A.K.A BWAN CHUCHU AFRIKI DUNIA


Mamia ya wananchi na wasanii nchini jioni hii wanahudhuria mazishi ya msanii maarufu wa Zanzibar Yusuf Ahmed Alley maarufu bwan’chuchu katika makaburi ya Mwanakwerekwe wilaya ya magharibi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari Marehemu Chuchu amefariki dunia mjini Nairobi, Kenya alikopelekwa kupatiwa matibabu baada ya kuugua kiasi ya mwezi mmoja uliopita.

Mwili wa msanii umerejeshwa mjini hapa ambapo taratibu za mazishi zilifanyika katika mtaa wa Kisima Majongoo na maziko yanafanyika jioni hii katika makaburi ya Mwanakwerekwe wilaya ya magharibi.


Marehemu Chuchu atakumbukwa kwa uhodari wake katika muziki hasa alipounda bendi ya Chuchu Sound iliyotamba kwa vibao vyake na chapuo za mazungumzo kati yake na Omari Mkali yaliyokuwa yakihitimishwa na neno la ‘ee! kwaheri’.

Marehemu chuchu pia alikuwa mmoja wa wajumbe wa bodi ya tamasha la kila mwaka la Sauti za busara na pia alikuwa anamiliki kituo cha redio cha Chuchu Fm kiliopo mjini hapa na studio ya kurekodia muziki.

Marehemu Chuchu aliefariki akiwa na umri wa miaka 51 ameacha mke mmoja ambae kwa sasa yuko nchini Marekani.

Uongozi wa Zenji Fm Radio unatoa mkono wa pole kwa familia ya marehemu pamoja na

Mungu amlaze mahali pema peponi AAMIN ndugu na jamaa na wafanyakazi wa CHUCHU FM RADIO

No comments:

Post a Comment