I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 2, 2010

KESI INAYOMKABILI MWENYEKITI WA DP YAENDELEA KUSIKILIZWA USHAHIDI

Mahakama ya hakimu mkaazi jijini Dar es salaam leo imesikiliza ushahidi wa kesi inayomkabili mwenyekiti wa chama cha DP mchungaji Kristopha Mtikila anaetuhumiwa kumkashifu rais Jakaya Kikwete mwaka 2007.
Katika ushahidi uliotolewa leo mahakamani hapo mkanda wa video uliokuwa na hutuba ya mtikila Mwezi Novemba mwaka 2007 eneo la mchikichini na kudaiwa kutoa maneno ya uchochezi yanayomkashifu Rais Kikwete .
Mara baada ya kuangaliwa kwa mkanda huo mahakamani hapo yaligunduliwa maneno ya uchochezi na Chuki zilizotolewa na Mtikila miongoni mwa maneno hayo ni kusema kuwa hawezi kuvumilia nchi kuongozwa na Muhuni.
Katika amaelezo yaliyotolewa na SP Muela ambae ni shahidi wa kwanza katika kesi hiyo ambapo mtikila alieleza kwamba yeye ni Mchungaji ,mwenyekiti wa DP na Raia wa Tanganyika maelezo ambayo wakili wa Mtikila alieleza kuwa Mteja wake maelezo hayo anayapinga na wala hakuyasema wala kuyaandika.
Mashahidi kadha awakiwemo waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali miongoni mwa mashahidi 10 wanatarajiwa kutoa ushahidi wao.

No comments:

Post a Comment