I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 2, 2010

WABUNGE NA WAWAKILISHI CUF WAMBWAGA KATIKA KURA ZA MAONI PEMBA

Baadhi ya Wabunge na wawakilishi waliopo madarakani katika majimbo mbali mbali Kisiwani Pemba wameendelea kuangushwa katika kura za maoni katika chama cha wananchi CUF .
Miongoni mwa wabunge ambao wameangusha katika kura hizo ni mbunge wa chakechake Fatma Magib alieyepata kura 417 dhidi ya mpinzani wake Mussa Haji Komba aliyepata kura 974.
Bunge mwengine ni Mbunge wa Jimbo la Chonga Rashid Chai aliepata kura 309 kwa kushindwa na Mohamed Juma Khamis aliyepata kura 414.
Wakati Mbunge wa Ziwani aliepo sasa hakujitokeza katika kinyanganyiro hicho na waliowania nafasi hiyo katika jimbo hilo ni Ahmed Juma Ngwali aliyepata kura 961 na kumshinda Yussuf Sharif aliyepata kura 90.
Kazi hiyo ya upigaji wa kura za maoni ulianza tarehe 21 Mwezi Mey mwaka huu na imemalizika jana katika jimbo la Konde.
Hata hivyo maamuzi ya mwisho ya kupitishwa wagombea wa nafasi hizo yatafanywa na baraza kuu la chama hicho June 15 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment