I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 2, 2010

ZANZIBAR:

Mkuu wa mkoa wa mjini Magharib Abdalah Mwinyi Khamisi amewataka maafisa na waratibu wa uandikishaji wa katika Daftari la wapiga kura linalosimamiwa na tume ya taifa ya uchaguzi NEC kusimamia vyema kazi hiyo katika kutoa haki kwa kila mwenyesifa ya kuandikishwa katika daftari.
Akizungumza katika mafunzo ya maafisa wa uandikishaji wa mkoa na ngazi ya majimbo yaliyofanyika katika Skuli ya Mbadala Rahaleo mjini Zanzibar.
Amewataka watendaji hao kutekeleza majukumu yao ya kitaifa kwa kutumia uzowefu watakao upata katika kusimamia vyema na kufanikisha zoezi hilo kufanyika kwa ufanisi.
Aidha amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuelimisha mawakala wao ili kufuata vyema taratibu za uandikishaji katika daftari la wapiga kura la NEC kwa lengo la kufanyika katika mazingira bora .
Nae Naibu Katibu wa uchaguzi wa tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania NEC Cotrida Komba amesema zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu upande wa Zanzibar Litaanza June 14 hadi 16 mwaka huu.
Aidha amewataka watanzania wote wenye sifa ya kundikishwa katika Daftari hilo ambao hawajaandikishwa na tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC kujitokeza kujiandikisha kwa mujibu wa taratibu ziliopo.

No comments:

Post a Comment