I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 2, 2010

BAADHI YA KERO ZA MUUNGANO ZAPATIWA UFUMBUZI NA SERIKALI YA MUUNGANO NA YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Kamati ya Pamoja ya serikali ya Muungano wwa Tanzania na ya Mapinduzi ya Zanzibar imetia saini hati ya makubaliano kuhusu kero za muungano zilizopatiwa ufumbuzi ikiwemo ile ya utekelezaji ya sheria za haki ya binaadam iliyokuwa haifanyi kazi Zanzibar na kuwekwa katika kero za Muungano .
Hati nyengine za kero za Muungano zilizotiwa saini ni utekelezaji wa sheria ya uvuvi katika eneo la bahari kuu ambayo pia ilikuwa katika kero za Muungano.
Kwa mujibu wa hati ya makubaliano utekelezaji wa masuala hayo umekamilika na si kero tena katika utekelezaji wa shughuli hizo na hivyo inapaswa kuondolewa katika ajenda za kamati hiyo ya pamoja

No comments:

Post a Comment