I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, June 1, 2010

VIKOSI VYA ULINZI NA USALAMA TANZANIA WAWASAKA MAHARAMIA WA KISOMALI WALIOKIMBILIA PEMBA

Vikosi vya ulinzi na usalama vimeripotiwa kuweko katika msako mkali wa kuwatafuta maharamia wa kisomali wanaodaiwa kukimbilia kisiwani Pemba baada ya kushindwa kuiteka meli katika bahari kuu ya Tanzania.

Kamanda wa polisi wa mkoa kusini Pemba Hassan Nassir amesema msako huo unavishirikisha vikosi vya SMZ na wanajeshi wa jeshi la wananchi Tanzania JWTZ.

Amesema taarifa za msako huo zitatolewa hapa baadae

Msako huo umekuja siku moja baada ya kuripotiwa watu wanaodaiwa maharamia waliotaka kuiteka nyara meli moja katika bahari ya Hindi upande wa Tanzania kukimbilia kisiwani Pemba.

Maharamia hao wamekimbilia Pemba baada ya kushambuliwa na majeshi ya jumuiya ya umoja wa ulaya wanaofanya doria katika pwani ya Afrika ya mashariki wakitaka kuiteka meli kati kati ya bahari ya visiwa vya Unguja na Pemba

No comments:

Post a Comment