I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 2, 2010

TUME YA UCHAGUZI ZNZ

Tume ya uchaguzi Zanzibar inakusudia kuwachukulia hatua za kisheria jumla ya wananchi 266 kwa madai ya kujiandikisha mara mbili katika Daftari la kudumu la wapiga kura.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Tume hiyo Salum Kassim ambapo amesema majina ya watu hao yatapelekwa katika afisi ya mkurigenzi wa Mashtaka Zanzibar ili kufikishwa mahakamani.
Akizungumza katika warsha ya waandishi wa habari juu ya masuala ya uchaguzi amesema uchaguzi wa mwaka 2005 watu wengi walijiandikisha mara mbili na wamepandikizwa na vyama vya siasa.
Hata hivyo hakutaja watu waliopandikizwa mwa 2005 lakini amesema tume mwaka huu imedhibiti wimbi hilo la upandikizaji.
Warsha hiyo kwa waandishi wa habari imeandaliwa na chama cha waandishi wa habari za maendeleo Zanzibar WAHAMAZA na Tume ya uchaguzi Zanzibar kwa kushirikiana na shirika la maendeleo ulimwenguni UNDP kupitia mfuko wa kusaidia uchaguzi Zanzibar .

No comments:

Post a Comment