I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, June 5, 2010

KERO YA WAFANYABIASHARA ZANZIBAR KUTOZWA KODI MARA MBILI YAPATIWA UFUMBUZI-WAZIRI KHATIB

Serikali za Tanzania zimekubaliana kuondoa usumbufu wa wafanyabiashara wa Zanzanzibar kutozwa kodi mara mbili wakati wanaposafirsha bidhaa zao kwenda Tanzania bara.

Makubaliano hayo yalifikiwa katika kikao cha kamati za kutatua kero muuungano kilichowashirikisha baadhi ya mawaziri wa serikali Mapinduzi Zanzibar na serikali ya muungano wa Tanzania katika hoteli ya Bwawani mapema wiki hii.

Akizungumza na Zenji Fm radio waziri anaeshughulikia masuala ya muungano Mohammed Seif Khatiba amesema chini makubaliano hayo mizigo ya wafanyabiashara itakayokuwa chini ya kiwango cha kulipia kodi afisa wa TRA alieruhusu mzigo huo kupita ndio atakae wajibika.

Amesema kabla ya makubaliano hayo wafanya biashara kutoka Zanzibar walikuwa wakitozwa kodi mara mbili kutokana na mizigo mizigo wanayosafirisha kwenda Tanzania bara kuwa chini ya kiwango cha kulipia kodi………CLIPS…….(SAVED-KHATIB)

Tatizo la wafanyabiashara Zanzibar kutozwa kodi mara mbili ni la muda mrefu na kukwamisha shughuli zao za biashara limefanywa kuwa agenda ya kero za muungano ambalo imepatiwa ufumbuzi.

No comments:

Post a Comment