I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, June 19, 2010

MSAMAHA WA KIKWETE HAUHUSU WAFUNGWA WA ZANZIBAR-SMZ

erikali ya mapinduzi Zanzibar imesema msamaha wa wafungwa unaotolewa na rais wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania hauhusu wafungwa walioko katika vyuo vya mafunzo vya Zanzibar.

Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi waziri wa nchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma amesema kila upande wa muunganoi una mamlaka yake , hivyo rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ndio mwenye mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa walioko Zanzibar na rais wa mungano anatoa msamaha kwa wafungwa walioko Tanzania bara.

Amesema licha ya Tanzania kuwa na mahakama moja ya rufaa inayoziunganisha nchi zote mbili, lakini wananchi watakaopatikana na hatia na kupewa adhabu ya kifungo wafungwa watapewa misahama kwa majibu wa mamla wa nchi hizo mbili.

Nae waziri kiongozi Shamsi Vuai Nahodha akiongezea majibu ya suala hilo amesema katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na katiba ya Zanzibar kuna mgawanyo maalumu ya mamlaka kulinga na makubaliano ya pande mbili za muungano.

Hivyo hivyo amesema serikali haitapanua wigo ambao unaweza Zanzibar kunyimwa mamlaka yake

No comments:

Post a Comment