I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, June 1, 2010

SMZ KUSHAURIWA KUACHANA NA KODI ZA SIGARA


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeshauriwa kutafuta njia mbadala za kuingiza mapato ili kuondokana na mapato yatokanayo na kodi za makampuni ya siraga kutokana kuhatarishs afya za watumiaji.

Akizungumza na Zenji fm radio juu ya siku ya kukataza uvutaji wa sigara duniani afisa wa elimu wa kitengo cha dawa za kulevya Zanzibar Dr. Kassi Ali Simai amesema hasara inayotokana na sumu ya sigara kwa afya ya mwadamu ni kubwa ikilinganishwa na mapato hayo.

Amefahamisha licha ya serikali kukusanya mapato mengi kutoka makampuni ya sigara, lakini moshi wake una zaidi ya chemical 400 zinazohatarisha afya za watumiaji hivyo ni vyema kufikiria njia nyingine mbadala ya ukusanyaji wa mapato.

Dr. Simai amesema vijana wengi wamekuwa wakiathirika na moshi wa sigara kwa kuugua homa ya ini na saratani

Katika kuadhimisha siku ya uvutaji wa sigara duniani shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO, limevilaumu viwanda vya sigara kwa kuwahamasisha wanawake katika nchi masikini kuvuta sigara.

Mtaalamu wa shirika hilo la WHO, Douglas Bettcher amesema, utafiti umeonesha idadi ya wanawake na vijana wanaovuta sigara katika nchi masikini imekuwa ikiongezeka.

No comments:

Post a Comment