I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, June 6, 2010

ZANZIBAR:

Katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha Mapinduzi CCM, Vuai Ali Vuai amesema mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho umechochea kasi ya maendeleo ya wananchi.
Amesema katika kipindi cha mwaka 2005/2010 serikali ya Mapinduzi Zanzibar imefanikiwa kutekeleza ilani hiyo na kutoa changamoto kwa wananchi kuongeza kasi ya uzalishaji kupitia miradi yao mbali mbali.
Akizunguma katika semina ya makatibu wa wilaya, uenezi na wana CCM wa wilaya za Unguja amesema sekta za maendeleo ya uchumi na kijamii zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kuwawezesha wananchi kupambana na umasikini.
Amesema miradi kama vile ya MACEMP, PADEP pamoja na miundo mbinu ya usambazaji wa maji, umeme na utowaji wa mafunzo umewasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi

No comments:

Post a Comment