I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, September 26, 2010

PROFISA LIPUMBA APATA AJALI TANGA

Msafara wa mgombea urais wa jamhuri ya muungano Tanzania kupitia chama cha wananchi CUF Profisa Ibrahim Harouna Lipumba umepata ajali leo asubuhi mkoani Tanga.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Handeni imehusisha magari mawili ya yaliokuwa katika kampeni, moja ilimbeba meneja wa kampeni na mgombea urais Profisa Lipumba na nyingine jingine limewabeba wandishi wanne wa habari.

Ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo la mgombea kuchomoka tairi na kupoteza mwelekeo. Hata hivyo mgombea huyo na meneja wa kampeni Saidi Miraj hawakupata majeraha, lakini walikimbizwa hospitali kwa ajili ya kuangaliwa afya zao.

Gari ya waandishi wa habari wanne ilipinduka mara mbili, lakinihakuna mwandishi hata mmoja aliepata majeraha makubwa

No comments:

Post a Comment