I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, September 10, 2010

KATIBU MKUU WA CUF HAMAD AMSIFU RAIS KARUME KWA KUIACHA ZANZIBAR KUWA NA AMANI

Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Seif Sharif Hamad, amesifu juhudi za rais wa Zanzibar Dr. Amani Abeid Karume, anaeondoka madarakani kwa kuiacha Zanzibar kuwa nchi ya amani.

Amesema busara za rais Karume katika kusimamia maridhiano ya kisiasa, zinahitaji kupongezwa kwa vile zimesababisha kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa, mara baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba 31 mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kumaliza sherehe za baraza la Edil fitr huko Forodhani, Hamad pia amesifu maendeleo ya kiuchumi yaliofikiwa na serikali ya rais Karume, katika ujenzi wa miundo mbinu ya kiuchumi na kijamii…

Kuhusu uendeshaji wa kampeni za kisiasa kwa ajili ya uchaguzi mkuu, katibu mkuu huyo amewataka viongozi wenzake wa kisiasa kuendesha kampeni za kistaarabu, ili kuenzi umoja na mshikamno wa wazanzibari uliopo.

No comments:

Post a Comment