I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

TANZANIA YATAKIWA KUBADILISHA KATIBA

Mgombea wa urais wa Jamhuri ya muungano Tanzania kupitia chama cha wananchi CUF Profia Ibrahim Harouna Lipumba amesema wakati umefika kwa watanzania kurekebisha katiba ili kuruhusu mgombea binafsi na kupanua wigo wa demokrasia nchini.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni wa chama hicho kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mjini Dar es Salaam Profisa Lipumba amesema kutokuwepo kwa fursa hiyo kunanyima mianya ya demokrasia na kuwacha watu wenye sifa za kuongoza kutokana na kutojiunga na vyama vya siasa.

Aidha Profisa Lipumba amesema endapo atachaguliwa kuwa rais amesema atapunguza umasikini unaowakabili watanzania……

Hii ni mara ya nne kwa profisa Lipumba kuwania urais wa Jamhuri ya muungano Tanzania kupita CUF tangu mfumo wa vyama vingi kuanza mwaka 1992.

No comments:

Post a Comment