I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, August 5, 2010

ZANZIBAR KUUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

Wananchi wa Zanzibar wamekubali muundo mpya wa serikali ya umoja wa kitaifa baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu kufuatia kupiga kura ya maoni ya ndio kwa asilimia 66.4 iliyofanyika jana.
Akitangaza matokeo hayo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar Khatib Mwinyichande amesema wananchi waliopiga kura ya ndio ni laki moja, 88 elf, 705 sawa na asilimia 66.4.
Kura za hapana ni elfu 95, 613 sawa na asilimia 33.6, kura zilizoharibika ni elfu nane 721 sawa na asilimia 3.0 kati ya wananchi waliopiga kura laki mbili, elfu 93 na 36 sawa na asilimia 71.9.
Kwa mujibu wa matokeo hayo Mwinyichande amewatangaza wananchi waliopiga kura ya ndio wameshinda katika kura ya maoni kwa asilimia 66.4…

Akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kutolewa matokeo hayo hoteli ya Bwawani katibu mkuu wa CUF Seif Sharif Hamad amesema kura hiyo inaonesha wazanzibar wametaka kusahau yaliopita.
Amesema ushindi huo ni wa wazanzibari wote na kwamba matumaini yake ni kuanza ukurasa mpya kwa kuijenga Zanzibar mpya na kuwataka wananchi kushirikiana ili kuiletea maendeleo nchi yao….
Nae naibu katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Saleh Ramadhan Ferouz amesema matokeo hayo yametoa picha juu ya wazanzibari wanaotaka kuungana katika kuijenga Zanzibar.
Aidha amewataka wananchi kuufanya uchaguzi mkuu

No comments:

Post a Comment