I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 2, 2010

WATU 20 WAHOFIWA KUFA MAJI MTWARA


Zaidi ya watu 20 wanahofiwa kufa maji mkoani Mtwara baada ya mashua waliokuwa wakisafiria kuzama baharini.

Mashua hiyo inayokadiriwa kuwa na watu 28 imezama leo mchana karibu na pwani ya mji wa Mtwara.

Kamanda wa polisi wa mkoa huo amesema hadi sasa mtu mmoja amekufa kati ya wanane waliokolewa na wengine 20 hawajulikani waliko Habari zinasema wakati waokowaji wakiendelea na shughuli za uokozi mmiliki wa mashua hiyo amekimbia pamoja na nahodha wake.

No comments:

Post a Comment