I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 4, 2010

KWANINI TANZANIA IMECHELEWA KUANZISHA VYUO VIKUU?


Imeelezwa kuwa sababu za Tanzania kuchelewa kuanzisha vyuo vikuu ni ubeberu wa kikoloni ambao ulikuwa hauwapendelei waafrika na maendeleo yao.
Akizungumza na Nyota Matukio Mwenyekita wa MISA TANZANIA ambae pia ni mhadhiri katika shule ya Habari na mawasiliano ya Umma (SJMC) Bw Ayoub Rioba amesema kuwa sababu hizo ndizo zilizopelekea kuchelewa kuanzishwa kwa vyuo vikuu vinavyotoa shahada za uandishi wa habari.
Rioba amesema kuwa kutokana na kuanzishwa kwa vyuo vikuu nchini vinavyotoa shahada kwa waandishi wa habari kumepelekea baadhi ya matatizo kuondoka kwa mujibu wa tafiti ziliofanywa zinazoonesha kuwa uandishi wa habari unazidi kuboreka.
Aidha Bw Rioba ametoa changamoto kwa waandishi wa habari kuweka maslahi ya taifa mbele.Katika mahojiano yake na Zenj fm Rioba alianza kwa kueleza sababu zilizopelekea kuchelewa kuanzishwa vyuo vikuu vya habari nchini vinavyotoa shahada kwa waandishi wa habari.. Bonyeza HAPA kusikiliza

No comments:

Post a Comment