I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 20, 2010

TCU IMEKIRI KUWEPO TATIZO LA USAJILI WA WANAFUNZI WANAOJIUNGA NA MASOMO KATIKA VYUO VIKUU NCHINI

Afisa habari kutoka tume ya vyuo vikuu nchini TCU Edward Mkaku amekiri kuwepo tatizo la usajili wa wanafunzi wanaojiunga na masomo katika vyuo vikuu nchini.
Bw Mkaku amesema moja ya matatizo katika usajili huo ni mtandao unaotumika katika utumaji maombi ya kujiunga na elimu hiyo kushindwa kumudu wimbi kubwa kutoka kwa wanafunzi wanaotumia huduma hiyo.
Akizungumza na shirika la utangazaji Tanzania Mkaku amesema Tume ya vyuo Vikuu inachukulia suala hilo kama changamoto ya maendeleo ya teknlojia na mawasiliano hususani katika kupunguza gharama kwa watumiaji.

No comments:

Post a Comment