I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 2, 2010

CHADEMA KUTUMIA BILIONI TANO KAMPENZI ZA UCHAGUZI MKUU 2010


Katibu mkuu wa chama cha maendeleo na Demokrasia CHADEMA Dr. Wilbord Slaa amesema chama hicho kinatarajia kutumia shilingi bilioni tano katika kampeni zake za uchaguzi mkuu utakaofanyika Octomba mwaka huu

Dr. Slaa amesema hayo alipokuwa akitangaza maamuzi ya kikao cha kamati kuu ya chama hicho kwa waandishi wa habari mjini Dar es Salaam.

Amesema kamati hiyo imepokea makadirio ya bajeti kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na kuelekeza sekritarieti ya chama hicho kuendelea kuipitia kwa kufuatilia vyanzo vya mapato.

No comments:

Post a Comment