I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 20, 2010

LIPUMBA ASEMA ZANZIBAR HUENDA IKAKOSA NAFASI KUNUFAIKA KIUCHUMI KATIKA SOKO LA PAMOJA LA JUMUIYA YA AFRIKA YA MASHARIKI


Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF, Profisa Ibrahim Haruna Lipumba amesema Zanzibar huenda ikakosa nafasi kunufaika kiuchumi katika soko la pamoja la jumuiya ya Afrika ya mashariki kutokana na kukosa viwanda vya uzalishaji wa bidhaa.
Profisa Lipumba ambae ni mchumi ameiambia Zenji Fm radio kwamza ili kuondokana na hali hiyo Zanzibar inahitaji kuweka miundo mbinu ya kuanzisha viwanda vitakavyotoa bidhaa mbali mbali ili kuuza katika soko hilo…
Hata hivyo amesema Zanzibar bado inahitajika kuzisindikiza taasisi za fedha na benki zinazotoa mikopo kwa kuweka masharti na riba nafuu kwa wafanyabiashara.
Jumuiya ya Afrika ya mashariki iliyoanzisha mwaka 1999 tayari imeshatekeleza itifaki za ushuru wa forodha, soko la pamoja na baadae inatarajiwa kutumia sarafu ya pamoja na hatimae kuwa shirikisho la kisiasa.

No comments:

Post a Comment