I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 2, 2010

BARA LA AFRICA LINAHITAJI TEKNOLOJIA ILI KUPIGA HATUA ZA MAENDELEO-KIKWETE


Rais Jakaya Kikwete amesema bara la Afrika linahitaji teknolojia ya kisasa kutoka nchi zinazoendelea kama vile Japan ili kuondoa tofauti kubwa kati ya nchi za Afrika na nchi zilizopiga hatua za kimaendeleo.

Rais Kiwete amesema hayo mjini Arusha wakati akifungua mkutano wa siku mbili unaowahusisha wafanyabiashara na mawaziri wa biashara kutoka Afrika

Amesema kama Afrika haitasaidia kiteknolojia kuna hatari kwa nchi nyingi kutofikia malengo ya millenium kufikia mwaka 2015.

Malengo ya mkutano huo ni kufuatilia utekelezaji wa mkutano wa nne wa wakuu wa nchi za Afrika na Japan uliozinduliwa mwaka 1993 nchini Japan.

Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na makundi ya biashara kutoka nchi mbali mbali za Afrika na wawakilishi kutoka Japan

No comments:

Post a Comment