I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 11, 2010

C U F

Chama Cha Wananchi CUF kimesema pamoja na kumalizika kwa daftari la kudumu la wapiga kura kiasi cha wananchi elfu 16 wenye haki na sifa za kuandikishwa hawakuandikishwa.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho Juma Said Sanani alipokuwa akizungumza na Zenji Fm Radio huko Afisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Amesema wananchi wengi ambao wamekosa kuandikishwa kutokana na sababu za kutokuwa na vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi na wengine kukosa vyeti vya kuzaliwa pamoja na barua za Masheha……CLIP(SANANI).
Tume ya uchaguzi Zanzibar imesema imefunga rasmi kazi za uwandikishaji wa wapiga kura na kuendelea na matayarisho ya uchaguzi baada ya kukamilika kwa kazi za uandikishaji, na ubadilishaji wa shahada za kupigia kura tume hiyo inaendelea na kazi za uhakiki wa majina ya wapiga kura waliosajiliwa katika awamu zote mbili.

No comments:

Post a Comment