I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 6, 2010

MKUTANO WA UCHUMI WA DUNIA,UTAWEZA KUFANIKIWA KUINUA UCHUMI WA AFRIKA IWAPO UTAANGALIA UWEZO WA MFUMO WA UZALISHAJI


Mkutano wa Uchumi wa Dunia,utaweza kufanikiwa kuinua uchumi wa Afrika iwapo utaangalia uwezo wa mfumo wa Uzalishaji
Ikiwa katika siku yake ya pili ya Mkutano wa Uchumi Duniani (WEF), ambao unawakutanisha washiriki kutoka nchi 85 duniani ,ukijadili namna ya kunyanyua uchumi wa Bara la Afrika hasa baada ya kukumbwa na msukosuko mwaka mmoja uliopita.
Wasomi hapa nchini wana maoni gani juu ya mkutano huo na ni kweli unaweza kufanikiwa katika kunyanyua Uchumi barani Afrika.
Mwangaza wa habari umemtafuta Daktari wa mambo ya uchumi ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk.Kasoga ,ambapo yeye amesema Mkutano huo unaweza kufanikiwa iwapo wataangalia uwezo wa mfumo wa kuzalisha uchumi wa Afrika
Hata hivyo, Mkutano huo unakusudia kutoa changamoto na mapendekezo ya njia sahihi ya kupambana na kutokomeza kabisa ugonjwa wa malaria ambao unadaiwa kuwa ni namba moja kwa kusababisha vifo vya kina mama waja wazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano duniani.

No comments:

Post a Comment