I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, May 23, 2010

ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewataka wananchi wanaofuga chui kujitokeza hadharani na wanyama hao ili kusaidia ukuwaji wa sekta ya utalii nchini.
Mkuu wa hifadhi ya msitu wa Jozani mkoa wa kusini Unguja Ali Mwinyi amesema serikali haiwakatazi wananchi wake kufuga chui iwapo wanayama hao wanawatumia kwa nia njema.
Amefahamisha Zanzibar inaendelea kuimarisha sekta ya utalii hivyo wanyama aina ya chui ni moja wapo ya vivutio kwa watalii na kwamba kuwepo hadharani kwa wanyama hao ni sawa na kuwepo hoteli ya nyota tano…
Mwinyi amesema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa katika miaka ya 90 umeonyesha chuwi wengi waliopo katika kisiwa cha Unguja asilimia 60 wanafugwa na wananchi na waliosalia wanaishi msituni.
Wananchi wa Zanzibar wanaamini watu wanafuga chui kwa imani za kishirikina, hivyo kauli hiyo ya serikali iliyotolewa miaka kadhaa iliyopita haiwezi kuleta mafanikio iwapo elimu zaidi haitatolewa.

No comments:

Post a Comment