I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 11, 2010

MICHEZO

Timu ya Majimaji ya Tumbe imefanikiwa kujinga na timu ya Falcon zote za Pemba kucheza ligi ya daraja la kwanza taifa msimu ujao baada ya kuichapa timu ya Azimio ya Mbuzini mabao 2-1 katika mchezo wa ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba.
Mchezo huo mzuri na wa kuvutia ulifanyika katika kiwanja cha Gombani Pemba.
Shirikisho la soka duniani FIFA limethibitisha kuongezea Afrika ya kusini zaidi ya dola mia moja na 50 za Marekani katika kuiwezesha nchi hiyo kukamilisha martayarisho ya michuano ya kombe la dunia.
Pesa hizo zitasaidia kutumika kakamilisha kambi za mazoezi kwa timu 32 zitakazaoshiriki.
Ikiwa imebakia mwezi mmoja kabla ya mashindano hayo kuanza wandishi wa habari wamesema yataipatia faida nchi ya Afrika ya kusini zaidi ya dola bilioni tatu kupitia hati ya kutangaza mashindano hayo kwa mashirika ya televisheni na udhamini.
Faida hiyo imelezewa ni kubwa zaidi kuwahi ikilinganishwa na nchi za awali zilizoandaa mashindano hayo, huku ikiwa nusu ya tiketi za mashindano hayo zikiwa zimeshauzwa.

No comments:

Post a Comment