I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 11, 2010

TUCTA

Katibu mkuu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA Nicolas Mgaya amesema azma ya kufanyika mgomo wa wafanyakazi nchi nzima iko pale pale na kinachosubiriwa ni kutolewa kwa baraka za mgomo huo na baraza kuu la shirikisho hilo.
Amesema baada ya mazungumzo ya tarehe nane mwezi huu kati yao na serikali majibu yatapelekwa kwenye baraza kuu litalofanyika ndani ya mwezi huu ambalo litakalotoa uwamuzi wa kufanyika mgomo huo au la.
Kwa upande mwengine pamoja na tangazo la waziri wa kazi na maendeleo ya vijana Juma Kapuya alilotoa April 30 juu ya kupanda kwa kima cha chini cha mishahara katika sekta binafsi kwa asilimia 100 kaimu katibu mkuu wa wizara hiyo amesema bado kuna kasoro kadhaa zinazohitaji marekebisho.

No comments:

Post a Comment