I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, May 20, 2010

COSOZA YAVAMIA MADUKA YA KASETI LEO

Afisi ya haki miliki imefanya msako maalum katika madula yanayokodisha na kuuza kanda za kazi za wasanii ambayo hayajafanya malipo ya kuuza kazi hizo za wasanii.
Akizungumza katika msako huo msimamizi na mtendaji mkuu wa afisi hiyo Mtumwa Khatib Khamis amesema lengo lao ni kuhakikisha haki za wasanii na wabunifu zinalindwa.
Amesema biashara ya sanaa imekuwa ikiwanufaisha wafanyabiashara pekee lakini wabunifu wanofanya kazi hiyo kama vile mziki, maigizo na sanaa za maumbo.
Msimamizi huyo amesema afisi yake imetoa elimu ya kutosha kwa wananchi na wanyabiashara wanaotumia kazi za sanaa kwa muda wa miaka mitatu sasa ili kujisajili na kufanya malipo lakini baadhi yao wameonekana kudharau juu ya hatua hiyo
Msako huo umefanyika katika maeneo ya Amani,Mpendae, Meli nne na tano barabara ya kuelekea Fuoni, Kwa Alinatuu na mali zilizokamatwa zinatarajiwa kuangamizwa na afisi hiyo.
Jumla ya wafanyabiashara wa maduka ya kanda 65 wamejisajili katika afisi hiyo kati ya hao wafanyabishara watano tuu ndio waliolipa kazi za sana hiyo.

No comments:

Post a Comment