I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, May 4, 2010

KISIWA CHA PEMBA

Baada ya Sakata la Mwakilishi wa jimbo la Tumbe Mh Ali Mohd Bakar aliyedaiwa kumpiga ngumi muuza samaki hivi karibuni kuingia katika hali nyingine ambayo inaonekana kuwastaajabisha wengi, hatimae mwakilishi huyo ameibuka na kudai kuwa vyombo vya habari havikumfanyia haki kwa kutangaza habari hizo pasi na kuulizwa.
Hata hivyo Nyota matukio ilipomthibitishia kuwa ilimtafuta kwa juhudi zake zote kuweza kujua kwa upande wake suala hili likoje aligeuka na kumtupia lawama mwandishi wetu aliyetoa taarifa hizi kwa mara ya kwanza kupitia Zenj fm Radio.
Aidha mwakilishi huyo pia alidai kuwa hakumshambulia mchuuzi wa samaki Said Kombo kama ilivyodaiwa hapo awali na badala yake ni yeye ndie aliyeshambuliwa na aliweka taarifa katika kituo cha polisi cha Chake chake na Bw alikwenda katika kituo cha polisi cha Wete wakati yeye alikuwa tayari ameshatkiwa. Bonyeza hapa kusikia Tukio Hilo

No comments:

Post a Comment